Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/02 uku. 8
  • Uwe Mwasiliani!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uwe Mwasiliani!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari Zinazolingana
  • Yehova Na Kristo Wawasilianaji Mashuhuri
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Uwasiliano Katika Huduma Ya Kikristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Kuwasiliana Ndani Ya Familia Na Katika Kundi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Mawasiliano Yenye Kujenga—Ufunguo wa Kuwa na Ndoa Nzuri
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 8/02 uku. 8

Uwe Mwasiliani!

1 Ili kutimiza utume wetu wa kuhubiri na kufanya wanafunzi, lazima tuwapashe wengine habari. (Mt. 24:14; 28:19, 20) Inaweza kuwa vigumu hata kwa marafiki kuwasiliana. Ni nini kinachoweza kutusaidia tuwasiliane vizuri na watu tusiowajua?

2 Kumfanya Mwenye Nyumba Akuone Kuwa Rafiki Wala Si Mgeni: Jaribu kujiweka katika hali ya wale unaowahubiria. Katika ulimwengu wa leo, inaeleweka kwamba wengine wanashuku, au hata kuogopa wageni. Hilo laweza kuzuia mazungumzo. Unaweza kushindaje wasiwasi wa wale unaokutana nao? Kabla hata hatujasema neno lolote, tunaweza kuwasiliana na watu kupitia sura yetu na mavazi yetu yenye kiasi. Mavazi yetu yenye kupendeza na mtazamo wetu wenye utulivu husaidia kuondoa woga.—1 Tim. 2:9, 10.

3 Msaada mwingine wa kuwasiliana ni kuwa watulivu na wenye urafiki. Hiyo husaidia kufanya wengine watulie na kuwafanya watake kusikiliza. Ili tuwe watulivu na wenye urafiki ni lazima tujitayarishe vizuri. Mara nyingi wasiwasi wetu hupungua ikiwa tunajua vizuri mambo tunayotaka kusema. Na utulivu huu wa akili hufanya wengine wavutiwe na ujumbe wetu. Mwanamke mmoja alisema hivi baada ya Shahidi mmoja kumtembelea: “Jambo moja ambalo nakumbuka kuhusu uso wake wenye tabasamu ni ile amani. Nilishangaa sana.” Hiyo ilifungua njia kwa mwanamke huyo kusikiliza habari njema.

4 Sifa Zinazovutia: Twahitaji kupendezwa na masilahi ya wengine. (Flp. 2:4) Njia moja ya kufanya hivyo ni kwa kuepuka kutawala mno mazungumzo. Mawasiliano hutia ndani kusikiliza. Tunapowaomba wasikilizaji wetu watoe maoni yao na kuwasikiliza kwa makini, wao huona kwamba twawajali. Kwa hiyo, watu hao wanapoongea, usiharakishe kueleza utoaji uliotayarisha. Wapongeze kwa unyofu ikiwezekana, na ujaribu kuendeleza mazungumzo kulingana na yale wanayosema. Maelezo yao yakionyesha yaliyo moyoni mwao, rekebisha utoaji wako ili uhusu mahangaiko yao.

5 Kiasi na hali ya akili ya kujishusha huendeleza mawasiliano. (Mit. 11:2; Mdo. 20:19) Watu walivutiwa na Yesu kwa sababu alikuwa “mwenye tabia-pole na wa hali ya chini moyoni.” (Mt. 11:29) Kwa upande mwingine, hali ya kujiona kuwa bora kuliko wengine haivutii watu. Kwa hiyo, ingawa twasadiki kabisa kwamba tuna ukweli, twaepuka kwa hekima kuwalazimisha watu wafuate maoni yetu.

6 Vipi ikiwa mtu anataja mambo ambayo hayapatani na mafundisho ya Biblia? Je, tuna wajibu wa kumrekebisha? Hatimaye tutamrekebisha, lakini si lazima tujaribu kumrekebisha kwenye ziara ya kwanza. Mara nyingi inafaa kuendeleza maoni ambayo yanapatana na ya mtu tunayezungumza naye kabla ya kumwambia mafundisho ya Biblia ambayo huenda akaona vigumu kuyakubali. Hiyo inahitaji subira na busara. Paulo aliweka kielelezo chema kuhusu jambo hili alipowahubiria mahakimu wa Areopago.—Mdo. 17:18, 22-31.

7 Zaidi ya yote, upendo usio wa kibinafsi utatusaidia kuwasiliana vizuri na wengine. Kama Yesu, lazima tuwahurumie watu ambao ‘wamechunwa ngozi na kutupwa huku na huku kama kondoo wasio na mchungaji.’ (Mt. 9:36) Hilo hutuchochea tuwapelekee habari njema na kuwasaidia waipate barabara iongozayo kwenye uhai. Ujumbe wetu ni wa upendo, kwa hiyo na tuendelee kuusema kwa upendo. Tukifanya hivyo, twamwiga Yehova Mungu na Yesu Kristo, ambao ndio wenye uwezo mkubwa zaidi wa kuwasiliana ulimwenguni.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki