Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/03 uku. 1
  • Je, Nyumba Yako Inaweza Kutumiwa?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Nyumba Yako Inaweza Kutumiwa?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Habari Zinazolingana
  • Sanduku La Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Kwa Nini Funzo la Kitabu la Kutaniko Ni Muhimu?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Jinsi Ambavyo Mpango wa Funzo la Kitabu la Kutaniko Hutusaidia
    Huduma ya Ufalme—2007
  • Jinsi ya Kunufaika Kutokana na Kikundi Chako cha Utumishi wa Shambani
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 2/03 uku. 1

Je, Nyumba Yako Inaweza Kutumiwa?

1 Katika karne ya kwanza, Wakristo wengi waliruhusu nyumba zao zitumiwe kwa ajili ya mikutano ya kutaniko. (1 Kor. 16:19; Kol. 4:15; Flm. 1, 2) Makutaniko mengine leo hayana nyumba za kutosha kufanyia Mafunzo ya Kitabu ya Kutaniko na mikutano ya utumishi wa shambani. Hivyo, mafunzo mengine ya kitabu yanalazimika kuwa na wahudhuriaji 30 au zaidi, badala ya idadi inayopendekezwa ya watu 15.

2 Pendeleo la Pekee: Je, ungependa nyumba yako itumiwe kwa ajili ya Funzo la Kitabu la Kutaniko? Chumba cha kadiri, chenye mwangaza na hewa ya kutosha kinaweza kutumiwa. Kuwa na funzo la kitabu nyumbani mwako ni pendeleo la pekee kwa sababu funzo la kitabu ni mkutano wa kutaniko na ni mpango wa Yehova wa kuwafundisha watu wake. Wengi wamesema kwamba wamefaidika kiroho kwa kuruhusu nyumba zao zitumiwe kwa ajili ya mkutano huo.

3 Ukiona kwamba nyumba yako inafaa, usisite kuwajulisha wazee. Huenda wanatafuta nyumba zaidi. Ikiwa funzo la kitabu haliwezi kufanyiwa nyumbani mwako, vipi mikutano ya utumishi wa shambani? Hata ikiwa hakuna uhitaji sasa, wazee watathamini kujua kwamba nyumba yako inaweza kutumiwa. Huenda ukafurahia pendeleo hilo wakati ujao.

4 Kuonyesha Adabu: Sote tunapaswa kuheshimu mali ya mwenye-nyumba tunapokutana katika nyumba za faragha. Wazazi wanapaswa kuhakikisha kwamba watoto wao wanatulia katika chumba cha funzo bila kuranda-randa sehemu nyinginezo nyumbani. Tunapaswa pia kuwajali majirani na kuepuka kuwasumbua bila sababu.—2 Kor. 6:3, 4; 1 Pet. 2:12.

5 Waebrania 13:16 hutuhimiza tusisahau ‘kutenda mema na kushiriki vitu pamoja na wengine, kwa maana Mungu hupendezwa vema na dhabihu za namna hiyo.’ Kuruhusu nyumba yako itumiwe kwa ajili ya mkutano wa kutaniko ni njia nzuri ya kushiriki vitu pamoja na wengine na ‘kumheshimu BWANA kwa mali yako.’—Mit. 3:9.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki