Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/03 uku. 1
  • ‘Ifanyie Nafasi’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Ifanyie Nafasi’
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Habari Zinazolingana
  • Kuna Faida za Kukaa Bila Kuoa au Kuolewa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Tumia Vizuri Kabisa Useja Wako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Useja—Njia ya Maisha Yenye Kuthawabisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Wakati Useja Ni Zawadi
    Amkeni!—1995
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 4/03 uku. 1

‘Ifanyie Nafasi’

1 Siku moja Yesu alipokuwa akizungumza na wanafunzi wake kuhusu ndoa, alisema kwamba useja ni “zawadi.” Kisha akasema: “Acheni yeye awezaye kufanyia hilo nafasi alifanyie hilo nafasi.” (Mt. 19:10-12) Baada ya miaka kadhaa kupita, mtume Paulo aliandika kuhusu manufaa ya useja na akawatia moyo wengine wafuate mfano wake wa kubaki mseja. (1 Kor. 7:7, 38) Leo wengi ‘wameufanyia nafasi’ useja na wanafurahia manufaa yake. Ni yapi baadhi ya manufaa hayo?

2 Kutumika “Bila Kukengeushwa Fikira”: Paulo alijua kwamba useja ulimpa fursa ya kumtumikia Yehova “bila kukengeushwa fikira.” Vivyo hivyo leo, ndugu mseja anaweza kuweka mradi wa kuhudhuria Shule ya Mazoezi ya Kihuduma, na kwa ujumla mseja yuko huru zaidi kufanya upainia, kujifunza lugha nyingine, kuhamia kwenye eneo lenye uhitaji, kutumika Betheli, au kuwa na mapendeleo mengine ya pekee ya utumishi. Huenda akawa na wakati na fursa zaidi za kujifunza kibinafsi kwa kina, kutafakari na kusali kwa Yehova kutoka moyoni. Kwa kawaida mseja ana wakati zaidi wa kujitoa kuwasaidia wengine. Yote hayo ‘humfaidi mtu kibinafsi.’—1 Kor. 7:32-35; Mdo. 20:35.

3 Kumtumikia Mungu hivyo bila kukengeushwa fikira huthawabisha sana. Baada ya kutumika nchini Kenya kwa miaka 27, dada mmoja mseja aliandika hivi: “Nilikuwa na marafiki wengi sana na kazi nyingi ya kufanya! Tulifanya mambo pamoja [na] kutembeleana. . . . Niliweza kutumia uhuru zaidi wa useja kushiriki katika huduma zaidi, na hili limeniletea furaha nyingi sana.” Aliongezea hivi: “Mwaka baada ya mwaka, uhusiano wangu na Yehova umeimarika.”

4 Kuifanyia Nafasi: Yesu alisema kwamba zawadi ya useja yapasa kudumishwa “kwa sababu ya ufalme wa mbingu.” (Mt. 19:12) Kama zawadi nyinginezo, useja wapaswa kutumiwa ifaavyo ili ulete shangwe na manufaa. Kwa kutumia vizuri fursa za useja na kumtegemea Yehova awape hekima na nguvu, waseja wengi wameona umuhimu wa kufanyia nafasi zawadi hiyo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki