Kazi Yetu Kuu Ni Huduma ya Kikristo
1 Sote tuna kazi za aina mbalimbali ambazo ni lazima tufanye. Kuiandalia familia yetu mahitaji ni takwa la kimungu. (1 Tim. 5:8) Hata hivyo, kazi tunayofanya ili kutimiza takwa hilo la kimungu haipaswi kuwa muhimu kuliko kazi ya kuhubiri Ufalme na kufanya wanafunzi.—Mt. 24:14; 28:19, 20.
2 Yesu alituwekea kielelezo cha kufuata katika “kutafuta kwanza ufalme.” (Mt. 6:33; 1 Pet. 2:21) Ingawa alikuwa na vitu vichache vya kimwili, alikaza fikira zake zote katika kufanya mapenzi ya Baba yake. (Luka 4:43; 9:58; Yoh. 4:34) Alijitahidi kuhubiri katika kila fursa. (Luka 23:43; 1 Tim. 6:13) Aliwahimiza wanafunzi wake wawe na bidii hiyohiyo katika kazi ya mavuno.—Mt. 9:37, 38.
3 Kumwiga Yesu Leo: Tunaweza kuiga kielelezo cha Yesu kwa kujitahidi kuishi maisha sahili yanayokazia huduma ya Kikristo. Tukiwa na mahitaji ya maisha, na tutii ushauri wa Biblia wa kutoendelea kukusanya mali zaidi za ulimwengu huu. (Mt. 6:19, 20; 1 Tim. 6:8) Itakuwa vyema zaidi tukijitahidi kupanua kazi yetu ya kuhubiri. Ikiwa tutakabili hali ngumu, na tujitahidi kama Yesu alivyofanya, bila kuruhusu mahangaiko ya maisha yawe muhimu kuliko kazi yetu kuu ya kutangaza habari njema za Ufalme.—Luka 8:14; 9:59-62.
4 Hata wale walio na madaraka mengi hutanguliza kazi ya kuhubiri. Ndugu mmoja mwenye familia kubwa na kazi ya maana, anayetumika akiwa mzee katika kutaniko la Kikristo anasema hivi: “Naiona huduma kuwa kazi kuu maishani mwangu.” Dada mmoja painia anasema hivi: “Kufanya upainia ni muhimu sana kuliko kazi yoyote nzuri ya kuajiriwa.”
5 Na tufuate kielelezo cha Yesu licha ya hali zetu. Jinsi gani? Kwa kufanya huduma ya Kikristo iwe kazi yetu kuu.