Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/07 uku. 1
  • Mwige Kristo Katika Huduma Yako

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mwige Kristo Katika Huduma Yako
  • Huduma ya Ufalme—2007
  • Habari Zinazolingana
  • “Nifuateni, Nami Nitawafanya Kuwa Wavuvi Watu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Kazi Yetu Kuu Ni Huduma ya Kikristo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • “Habari Njema Lazima Zihubiriwe Kwanza”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • “Nendeni Mkafanye Wanafunzi”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2007
km 2/07 uku. 1

Mwige Kristo Katika Huduma Yako

1 Yesu aliweka mfano ambao tunapaswa kufuata katika huduma. Alionyesha mara nyingi na kwa njia nyingi kwamba alimpenda sana Mungu na wanadamu. Aliwafundisha wapole ukweli na kuwafanyia matendo mengi ya fadhili zenye upendo walioteseka na kukandamizwa.—Mt. 9:35.

2 Mfano wa Yesu na Mafundisho Yake: Yesu hakukengeushwa kwa kujihusisha katika mambo ya kisiasa au kutoa misaada ya kufaidi jumuiya. Pia hakuruhusu mambo mengine yamkengeushe au yachukue mahali pa kazi yake kuu. (Luka 8:1) Alikazia hasa kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu kuwa suluhisho pekee la kudumu kwa matatizo ya wanadamu. Yesu alikuwa na kazi ya maana sana lakini alikuwa na wakati mfupi tu wa kuifanya. Watu katika jiji la Kapernaumu walipotaka abaki huko, Yesu aliwaambia hivi wanafunzi wake: “Twendeni mahali pengine . . . ili nipate kuhubiri huko pia, kwa maana nilitoka kwa kusudi hilo.”—Marko 1:38.

3 Baada ya kuwazoeza wanafunzi wake, Yesu aliwatuma akiwapa maagizo haya hususa: “Hubirini, mkisema, ‘Ufalme wa mbinguni umekaribia.’” (Mt. 10:7) Aliwafundisha wafuasi wake kwamba masilahi ya Ufalme yanapaswa kuchukua mahali pa kwanza maishani. (Mt. 6:33) Maneno ya mwisho ambayo Yesu aliwaambia wanafunzi wake yaliwaonyesha wazi kazi waliyopaswa kufanya. Alisema: “Kwa hiyo nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote.”—Mt. 28:19.

4 Umuhimu wa Ufalme: Jambo kuu la mazungumzo ya Yesu lilikuwa Ufalme wa Mungu, naye aliwatia moyo wanafunzi wake wafuate mfano wake. Jitihada za wanadamu za kutatua shida zilizopo haziwezi kufaulu. (Yer. 10:23) Ni Ufalme wa Mungu tu utakaotakasa jina la Mungu na kuandaa kitulizo cha kudumu kwa wanadamu. (Mt. 6:9, 10) Tunapofundisha kuhusu Ufalme, tunawasaidia watu “wanaougua na kulia kwa sababu ya machukizo yote yanayofanywa” kuishi maisha yenye furaha na mafanikio sasa na kupata tumaini linalotegemeka la wakati ujao.—Eze. 9:4.

5 Bado Yesu anahusika katika kazi yetu ya kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu, naye anatuhakikishia kwamba atatutegemeza. (Mt. 28:20) Je, huduma yetu inapatana na kielelezo ambacho Yesu alituwekea? (1 Pet. 2:21) Katika siku hizi za mwisho zenye msukosuko, na tufanye yote tuwezayo kufuata kwa ukaribu mfano ambao Yesu alituwekea katika huduma!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki