Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/03 uku. 1
  • Kazi Ambayo Huburudisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kazi Ambayo Huburudisha
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Habari Zinazolingana
  • “Chukueni Nira Yangu”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • “Njooni Kwangu, . . . Nami Nitawaburudisha”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • ‘Kupata Burudisho la Nafsi Zenu’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • “Nira Yangu ni ya Fadhili na Mzigo Wangu ni Mwepesi”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 8/03 uku. 1

Kazi Ambayo Huburudisha

1 Ujumbe wa Biblia huburudisha wote ambao huukubali na kuutumia maishani mwao. (Zab. 19:7, 8) Ujumbe huo huwasaidia kuacha mafundisho ya uwongo na mazoea yenye kudhuru na hutoa tumaini lenye kutegemeka la wakati ujao. Hata hivyo, wale ambao hufaidika na habari njema si wale tu wanaozipokea. Wale ambao huwatangazia wengine kweli za Biblia zenye kuburudisha, huburudishwa pia.—Mit. 11:25.

2 Kutiwa Nguvu na Huduma: Yesu alisema kwamba wale wanaokubali kubeba nira ya kuwa wanafunzi wa Kristo, ambayo inatia ndani kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi, ‘wangepata burudisho kwa ajili ya nafsi zao.’ (Mt. 11:29) Yeye mwenyewe alitiwa nguvu kwa kuwahubiria wengine. Kufanya hivyo kulikuwa kama chakula kwake. (Yoh. 4:34) Alipowatuma wanafunzi 70 kuhubiri, walifurahi walipoona Yehova akiunga mkono jitihada zao.—Luka 10:17.

3 Wakristo wengi leo hutiwa nguvu pia wanaposhiriki katika kazi ya kuhubiri. Dada mmoja alisema: “Huduma inaburudisha kwa sababu huyafanya maisha yangu yawe na kusudi. Matatizo ya kibinafsi na mikazo ya kila siku hupungua ninaposhiriki katika utumishi.” Mhudumu mwingine mwenye bidii alisema: “Huduma . . . humfanya Yehova awe halisi kwangu kila siku na hunipa amani na furaha moyoni ambazo haziwezi kupatikana vinginevyo.” Tuna pendeleo lililoje la kuwa “wafanyakazi wenzi wa Mungu”!—1 Kor. 3:9.

4 Nira ya Kristo Ni Yenye Fadhili: Ingawa Wakristo wanahimizwa ‘wajikakamue wenyewe kisulubu,’ Yesu hadai mengi kuliko yale tunayoweza kufanya. (Luka 13:24) Kwa kweli, yeye hutualika kwa upendo ‘tuchukue nira yake.’ (Mt. 11:29) Wale ambao lazima wakabiliane na magumu wanaweza kuwa na hakika kwamba utumishi wao wa nafsi yote, hata ukiwa mdogo, unampendeza Mungu.—Marko 14:6-8; Kol. 3:23.

5 Ni jambo lenye kuburudisha kama nini kumtumikia Mungu ambaye anathamini lolote tunalofanya kwa ajili ya jina lake! (Ebr. 6:10) Na tujitahidi sikuzote kumpa yaliyo bora.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki