Tafadhali Watembelee Bila Kukawia
Uwatembelee nani bila kukawia? Wale wanaoomba wapelekewe vichapo au magazeti kwa ukawaida au wale ambao wangependa Shahidi awatembelee nyumbani kwao. Maombi hayo hutoka wapi? Hutoka kwa wale ambao huwasiliana na ofisi ya tawi kwa barua au simu au kupitia kituo chetu rasmi cha Internet. Ofisi ya tawi inapopokea maombi hayo, inalijulisha kutaniko la karibu kupitia fomu ya S-70 yenye kichwa “Tafadhali Pangeni Mhubiri Anayestahili Amzuru Mtu Huyu.” Mara wazee wanapopokea fomu ya S-70, wanapaswa kumpa mhubiri ambaye atajitahidi kumtafuta mtu huyo anayependezwa. Mhubiri akishindwa kumpata mtu huyo nyumbani, anaweza kujaribu kuwasiliana naye kwa simu au kuacha barua fupi mahali ambapo haionekani. Ukiombwa kumtembelea mtu anayependezwa, jitahidi kufanya hivyo bila kukawia.