Sanduku la Swali
◼ Ni nani anayepaswa kujaza kuponi na fomu ya maombi kwenye Intaneti?
Kwa kawaida, machapisho yetu yana kuponi ambazo zinaweza kujazwa na kutumwa kwa ofisi ya tawi ili kuomba machapisho au kutembelewa na Mashahidi wa Yehova. Kwa kuongezea, Tovuti yetu ya www.watchtower.org inaweza kutumiwa kuomba funzo la Biblia. Maandalizi haya yanawasaidia wengi kujifunza kweli. Hata hivyo, kumekuwa na matatizo wakati wahubiri wanapotumia vifaa hivi kufanya mipango kwa ajili ya watu wao wa ukoo au wengine ili wapokee msaada wa kiroho.
Wengine ambao wametumiwa machapisho ambayo hawakuomba kutoka kwa ofisi ya tawi wamelalamika, wakihisi kwamba tengenezo letu linawasumbua na limewaweka katika orodha fulani ya watu wanaotumiwa machapisho kwa ukawaida. Wahubiri ambao wamepata taarifa ya kumtembelea mtu fulani ambaye hakuomba atembelewe, wamejipata katika hali ya kutatanisha mtu huyo anapoonyesha amesumbuliwa. Kwa hiyo, maombi yanayofanywa katika Tovuti yetu au kupitia kuponi yanapaswa kutoka kwa wanaopendezwa wala si kutoka kwa wahubiri wanaotuma maombi kwa niaba ya wengine. Maombi yanapotambuliwa kuwa yametumwa kwa niaba ya mtu mwingine, kwa kawaida hayashughulikiwi.
Hivyo basi, tunaweza kumsaidiaje kiroho mtu wa ukoo au mtu tunayemfahamu? Ikiwa ungependa apokee machapisho, kwa nini usiyatume kwake moja kwa moja yakiwa zawadi? Iwapo anapendezwa na angependa kutembelewa na Mashahidi lakini hujui jinsi ya kuwasiliana na wazee wa kutaniko lililo karibu naye, jaza fomu ya Tafadhali Fuatia Upendezi (S-43) kisha umpe mwandishi wa kutaniko, ambaye ataipitia na kuituma kwa ofisi ya tawi. Hata hivyo, ikiwa anayependezwa yuko gerezani, au katika hospitali zinazoshughulikia watu walio na uraibu mbalimbali, usiwasiliane na ofisi ya tawi kwa niaba yake. Badala yake, unaweza kumtia moyo awasiliane na ndugu wanaotembelea makao hayo au yeye binafsi aiandikie ofisi ya tawi.