Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/15 uku. 2
  • Sanduku La Swali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sanduku La Swali
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Habari Zinazolingana
  • Matumizi ya Internet—Uwe Chonjo Kuhusu Hatari Zake!
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Sanduku la Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Internet—Kwa Nini Utahadhari?
    Amkeni!—1997
  • Huduma na Vyanzo vya Habari vya Internet
    Amkeni!—1997
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2015
km 7/15 uku. 2

Sanduku La Swali

◼ Je, wahubiri wanapaswa kutumia sana Intaneti ili kuwahubiria au kujifunza na watu wasiowafahamu wanaoishi katika nchi nyingine?

Wahubiri wengine wametumia Intaneti ili kupata mafunzo ya Biblia katika nchi ambazo kazi yetu iko chini ya vizuizi au katika nchi zenye wahubiri wachache. Katika visa fulani, kumekuwa na matokeo mazuri. Hata hivyo, kuna hatari wakati ambapo wahubiri wanawasiliana kupitia barua pepe au wanakuwa na mazungumzo kwenye mtandao na watu wasiowafahamu. (Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Julai 2007 uku. 3.) Ingawa kusudi ni kuwafikishia watu wenye moyo mnyoofu ujumbe wa habari njema ya Ufalme, mazungumzo hayo yanaweza kumfanya ndugu au dada ajihusishe na mashirika mabaya, kutia ndani waasi imani. (1 Kor. 1:19-25; Kol. 2:8) Kwa kuongezea, katika nchi ambazo kazi yetu ya kuhubiri iko chini ya vizuizi au imepigwa marufuku, mawasiliano hayo yanaweza kuchunguzwa na wenye mamlaka na hivyo kuhatarisha ndugu na dada wanaoishi katika nchi hizo. Kwa hiyo, wahubiri hawapaswi kutumia Intaneti ili kutafuta watu kutoka nchi nyingine kwa kusudi la kuwahubiria.

Isipokuwa kuwe na maagizo tofauti kutoka ofisi ya tawi, tunapomhubiria isivyo rasmi mtu tusiyemfahamu kutoka nchi nyingine, hatupaswi kuendeleza upendezi wake anaporudi nyumbani. Badala yake, tunaweza kumwonyesha jinsi ya kutumia Tovuti yetu ya jw.org ili apate habari zaidi au tumweleze jinsi anavyoweza kuwasiliana na ofisi ya tawi ya nchi yake. Pia, tunaweza kumtia moyo atembelee Jumba la Ufalme lililo karibu na eneo analoishi. Ni kweli kwamba katika nchi nyingine hakuna Majumba ya Ufalme. Ikiwa angependa kutembelewa na Mashahidi wanaoishi katika eneo lake, tunapaswa kujaza fomu ya Tafadhali Fuatia Upendezi (S-43) na kumpa mwandishi, ambaye ataituma kupitia Tovuti ya jw.org. Ofisi ya tawi inayosimamia kazi ya kuhubiri katika nchi ambayo mtu anayependezwa anaishi, inajua vizuri hali za pekee za eneo hilo na hivyo inaweza kutoa msaada wa kiroho unaohitajika.—Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Juni 2014, uku. 7, na Huduma Yetu ya Ufalme ya Novemba 2011, uku. 2.

Ikiwa mtu tunayejifunza naye anahamia nchi nyingine au ikiwa mtu ambaye tunajifunza naye wakati huu anaishi nchi nyingine na tunamfahamu kupitia Intaneti tu, tunapaswa kufuata mwongozo uliotolewa hapo juu. Hata hivyo, tunaweza kuendeleza upendezi wake hadi wahubiri walio kwenye eneo lake wawasiliane naye. Lakini, ikiwa anaishi katika nchi ambayo kazi yetu iko chini ya vizuizi au imepigwa marufuku, tunapaswa kuwa na tahadhari sana tunapozungumzia habari za Biblia kupitia barua, simu, au njia nyingine ya kielektroniki.—Mt. 10:16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki