Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/05 uku. 7
  • Sanduku La Swali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sanduku La Swali
  • Huduma ya Ufalme—2005
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi ya Kusaidia Baada ya Janga
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2023
  • Tunaweza Kusaidiaje?
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Ni Kazi Gani Zinazofanywa Katika Ofisi ya Tawi?
    Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Kutegemeza Kazi ya Ufalme Kwenu na Ulimwenguni Pote
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2005
km 1/05 uku. 7

Sanduku La Swali

◼ Ni njia gani bora ya kutoa michango ya kuwasaidia ndugu walio na uhitaji katika nchi nyingine?

Nyakati nyingine, tunasikia kwamba ndugu katika nchi fulani wamepungukiwa na vitu vya kimwili kwa sababu ya mateso, msiba, au magumu mengine. Baadhi ya ndugu wametuma pesa moja kwa moja kwenye ofisi za tawi katika nchi hizo na kuomba pesa hizo zitumiwe kumsaidia mtu, kutaniko, au mradi fulani wa ujenzi. —2 Kor. 8:1-4.

Hangaiko hilo lenye upendo kwa waamini wenzetu linathaminiwa sana, hata hivyo, mara nyingi kuna mahitaji yanayopaswa kushughulikiwa haraka zaidi kuliko yale ambayo yule anayetoa mchango anapendekeza. Nyakati nyingine, uhitaji uliotajwa na yule anayetoa mchango tayari umeshughulikiwa. Bila shaka tunaweza kuwa na uhakika kwamba michango inapotumwa kwenye ofisi ya tawi kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote, Hazina ya Majumba ya Ufalme, au kusaidia wakati wa msiba, hutumiwa kulingana na maagizo ya yule aliyetoa mchango.

Ndugu katika ofisi zote za tawi wamezoezwa kushughulikia kwa haraka mahitaji yasiyotazamiwa. Ofisi hizo hujulisha Baraza Linaloongoza kuhusu hali zote za dharura. Ikiwa msaada wa ziada unahitajika, Baraza Linaloongoza linaweza kuomba ofisi za tawi zilizo karibu zisaidie, au pesa zinaweza kutumwa moja kwa moja kutoka makao makuu.—2 Kor. 8:14, 15.

Kwa hiyo, michango yoyote inayotolewa kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote, miradi ya ujenzi katika nchi nyingine, au kusaidia wakati wa msiba, inapaswa kutumwa kwenye ofisi ya tawi ya nchi unayoishi, kupitia kutaniko, au moja kwa moja. Kwa njia hiyo, “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” hushughulikia kwa utaratibu mahitaji ya akina ndugu ulimwenguni pote kupitia mipango iliyowekwa na Baraza Linaloongoza.—Mt. 24:45-47; 1 Kor. 14:33, 40.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki