Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/05 uku. 6
  • Wasaidie Wapate Ushahidi Zaidi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wasaidie Wapate Ushahidi Zaidi
  • Huduma ya Ufalme—2005
  • Habari Zinazolingana
  • Kuwahubiria Watu Wanaozungumza Lugha ya Kigeni
    Huduma ya Ufalme—2009
  • Jinsi ya Kutumia Fomu ya Tafadhali Fuatia Upendezi (S-43)
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Njia za Kuhubiri Habari Njema
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Kuonyesha Hali ya Kutopendelea Katika Huduma Yetu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2005
km 2/05 uku. 6

Wasaidie Wapate Ushahidi Zaidi

1 Tunapohubiri habari njema, mara kwa mara sisi hukutana na watu ambao hawaishi katika eneo letu au wanaozungumza lugha ya kigeni, kutia ndani lugha ya ishara. Huenda wengine ambao tumekuwa tukizungumza nao kuhusu Biblia wakahamia eneo lingine. Tunawezaje kufanya mpango ili watu hao wapate ushahidi zaidi? Tunaweza kufanya hivyo kwa kutumia fomu ya Tafadhali Fuatia Upendezi (S-43-SW).

2 Mara nyingi, watu husikiliza habari njema kwa makini zaidi wanapohubiriwa katika lugha yao wenyewe. (Mdo. 22:1, 2) Hivyo, kwa kawaida tunapokutana na mtu anayezungumza lugha ya kigeni, tunapaswa kujaza fomu hiyo hata kama mtu huyo hapendezwi na ujumbe wa Ufalme. Hata hivyo, katika maeneo ambako kuna watu wengi wanaozungumza lugha ya kigeni na ambao huhubiriwa kwa ukawaida katika lugha yao, huenda isiwe lazima kujaza fomu hiyo isipokuwa tu upate mtu anayependezwa.

3 Kujaza Fomu Hiyo: Tumia busara unapomwuliza mtu huyo jina lake, anwani yake, na namba yake ya simu. Onyesha amependezwa kwa kadiri gani, wakati anapoweza kupatikana, kichapo alichoachiwa au alichoomba, na lugha anayoielewa vizuri. Baada ya kuijaza fomu hiyo, mpe mwandishi wa kutaniko bila kukawia, naye ataituma kwenye kutaniko au kikundi kinachoweza kumsaidia mtu huyo.

4 Kutuma Fomu Hiyo: Ikiwa mwandishi hana anwani au hajui kutaniko au kikundi kinachopaswa kupelekewa fomu hiyo, anaweza kupiga simu kwenye ofisi ya tawi na kuzungumza na Idara ya Utumishi inayoshughulikia maeneo ili apate habari anazohitaji. Si lazima kumjulisha mwangalizi wa jiji fomu hiyo inapotumwa.

5 Kutaniko au kikundi fulani kinapopokea fomu ya Tafadhali Fuatia Upendezi iliyojazwa, mipango inapaswa kufanywa bila kukawia ili kumtembelea mtu huyo. Tunapotimiza sehemu yetu kwa bidii, tunaweza kuwa na hakika kwamba Yehova atafungua mioyo ya wale wenye “mwelekeo unaofaa kwa ajili ya uzima wa milele.”—Mdo. 13:48.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki