Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/07 uku. 1
  • Kumwabudu Yehova Tukiwa Familia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kumwabudu Yehova Tukiwa Familia
  • Huduma ya Ufalme—2007
  • Habari Zinazolingana
  • Familia ya Kikristo Hufanya Mambo Pamoja
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Msaada kwa Familia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Kutangaza Habari Njema—Tukiwa Familia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Jinsi Ambavyo Washiriki wa Familia Hushirikiana ili Kushiriki Kikamili—Katika Huduma
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2007
km 8/07 uku. 1

Kumwabudu Yehova Tukiwa Familia

1 Katika nyakati za Biblia, washiriki wa familia walifanya mambo mengi pamoja. Walitimiza shughuli za kawaida wakiwa familia, lakini jambo la maana hata zaidi ni kwamba walimwabudu Yehova pamoja. (Law. 10:12-14; Kum. 31:12) Leo, katika maeneo mengi, washiriki wa familia hawafanyi mambo mengi pamoja. Hata hivyo, Wakristo wanatambua umuhimu wa kufanya mambo pamoja wakiwa familia, hasa mambo yanayohusu ibada. Bila shaka Mwanzilishi wa familia hupendezwa sana anapoona familia zikimwabudu kwa umoja!

2 Hubirini Pamoja: Kuhubiri habari njema pamoja huimarisha familia. Kwa hiyo, mbali na kuhubiri pamoja na wengine kutanikoni, mzee atahubiri pia na mke na watoto wake kwa ukawaida. (1 Tim. 3:4, 5) Licha ya kuwa na shughuli nyingi, hata waangalizi wanaosafiri hupangia wakati wa kuhubiri pamoja na wake zao.

3 Wazazi wanaohubiri pamoja na watoto wao hupata fursa ya kuwasaidia kufanya maendeleo wakiwa wahubiri. Watoto hawataona tu shangwe na uradhi wa wazazi wao katika huduma, bali pia wataona wazazi wao wakionyesha jinsi wanavyompenda Yehova na wanadamu wenzao. (Kum. 6:5-7) Umuhimu wa jambo hilo haupungui watoto wanapokuwa wakubwa. Wenzi fulani wa ndoa walio na wana watatu wenye umri wa kati ya miaka 15 na 21 wanaendelea kuhubiri pamoja nao kwa ukawaida. Baba yao alisema: “Kila wakati sisi huwafundisha jambo fulani, nasi tunahakikisha kwamba wanafurahia huduma na kutiwa moyo.”

4 Tayarisheni Pamoja: Familia zimepata faida kwa kujitayarisha pamoja kwa ajili ya huduma. Mara nyingi watoto hufurahia vipindi vya kufanya mazoezi ya kuhubiri. Katika vipindi hivyo, washiriki wa familia hupokezana zamu ya kuhubiri au ya kuwa wenye nyumba. Familia nyingine hutumia dakika chache mwishoni mwa funzo la familia kufanya hivyo.

5 Shangwe yetu huongezeka tunaposhiriki katika kazi muhimu na zenye kuridhisha pamoja na wale tunaowapenda. Inafurahisha kama nini washiriki wa familia wanapofanya kazi pamoja katika huduma ya shambani kwa kuhubiri nyumba kwa nyumba, kufanya ziara za kurudia, na kuongoza mafunzo ya Biblia! Ukimwabudu Yehova kwa njia hiyo pamoja na familia yako, unaweza kusema hivi kwa shangwe: “Mimi na nyumba yangu, tutamtumikia Yehova.”—Yos. 24:15.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki