Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/08 uku. 1
  • Tumia Wakati Vizuri Unapokuwa Shambani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tumia Wakati Vizuri Unapokuwa Shambani
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Habari Zinazolingana
  • Mikutano ya Utumishi wa Shambani Inayotimiza Kusudi Lake
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Mikutano ya Utumishi wa Shambani
    Huduma ya Ufalme—2009
  • Sanduku la Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Nufaika Kikamili na Mikutano ya Utumishi wa Shambani
    Huduma ya Ufalme—2006
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 1/08 uku. 1

Tumia Wakati Vizuri Unapokuwa Shambani

1 Kwa kweli kuna mengi ya kutimiza katika huduma yetu, na wakati uliobaki umepungua. (Yoh. 4:35; 1 Kor. 7:29) Tukiwa na ratiba nzuri na kujitayarisha mapema, tunaweza kutumia vizuri wakati tuliotenga kwa ajili ya huduma.

2 Jitayarishe: Kabla ya kwenda kwenye mkutano wa utumishi wa shambani, hakikisha kwamba una vichapo utakavyohitaji na umetayarisha jambo utakalosema shambani. Baada ya mkutano huo kufungwa kwa sala, nenda moja kwa moja kwenye eneo. Hilo litakuwezesha wewe na wale wanaoambatana nawe kutimiza mengi katika muda mliopangia kwa ajili ya utumishi wa shambani.

3 Ikiwa umewekwa rasmi kuongoza mkutano wa utumishi wa shambani, anza mkutano huo kwa wakati. Mkutano huo unapaswa kuwa mfupi, uwe kati ya dakika 10 hadi 15. Kabla kikundi hakijatawanyika, hakikisha kwamba kila mtu anajua atahubiri na nani na eneo atakalohubiri.

4 Unapokuwa Kwenye Huduma: Mara tu mkutano wa utumishi wa shambani unapomalizika, usikawie-kawie, nenda moja kwa moja kwenye eneo. Ikiwa unatarajia kuondoka mapema, fanya mipango yako mwenyewe ili wengine katika kikundi wasiondoke mapema kwa sababu yako. Unapohubiri, wajali wengine ambao huenda wakawa wanakungoja umalize mazungumzo. Unaweza kutumia busara na kukatiza mazungumzo na mtu mbishi au unaweza kupanga kumrudia mtu ambaye amependezwa.—Mt. 10:11.

5 Unapofanya ziara za kurudia, unaweza kuepuka kutumia wakati mwingi kusafiri kwa kuwarudia watu wote wanaoishi eneo moja kabla ya kwenda kwenye eneo lingine. Ikiwezekana, wapigie simu watu ambao unapanga kuwarudia ili ujue ikiwa wako nyumbani. (Met. 21:5) Ikiwa unatarajia ziara ya kurudia ichukue muda mrefu, wengine walio katika kikundi chako wanaweza kuhubiri hapo karibu au wafanye ziara nyingine ya kurudia.

6 Tunaishi wakati wa mavuno makubwa ya kiroho. (Mt. 9:37, 38) Kazi hiyo itamalizika hivi karibuni. Kwa hiyo, tamaa yetu inapaswa kuwa kutumia vizuri wakati wetu tunapokuwa katika huduma.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki