Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Desemba 1
“Je, umeona kwamba watu wana viwango vya usafi vinavyotofautiana? [Mruhusu ajibu.] Hapa kuna sababu moja inayoonyesha umuhimu wa usafi. [Soma 1 Petro 1:16.] Makala hii inatoa madokezo mazuri kuhusu kudumisha usafi.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 9.
Amkeni! Desemba
“Watu wengi hujitahidi kumtukuza Yesu wakati huu wa mwaka. Kulingana na andiko hili, ungesema ni njia gani bora ya kumtukuza Yesu? [Soma Yohana 14:15. Mruhusu ajibu.] Tarehe hususa aliyozaliwa Yesu haijulikani, na huenda ukashangaa kujua kwamba Desemba 25 ilichaguliwa tu kuwa tarehe ya kusherehekea Krismasi.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 10.
Mnara wa Mlinzi Januari 1
“Watu duniani kote wana maoni yanayotofautiana kumhusu Maria, mama ya Yesu. Wewe una maoni gani? [Mruhusu ajibu.] Biblia inaonyesha kwamba Maria alikuwa na jukumu la pekee katika historia. [Soma Luka 1:30-32.] Gazeti hili linazungumzia mambo tunayoweza kujifunza kutokana na mfano wake.”
Amkeni! Januari
“Maziwa na mito mingi duniani inakauka, na watu wengi hawawezi kupata maji safi ya kunywa. Je, unafikiri mwanadamu ana uwezo wa kutatua tatizo hili kabisa? [Mruhusu ajibu, kisha usome Yeremia 10:23.] Gazeti hili linazungumzia suluhisho pekee linaloonyeshwa katika Biblia.”