Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/09 uku. 2
  • Jinsi ya Kutayarisha Mkutano wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kutayarisha Mkutano wa Utumishi
  • Huduma ya Ufalme—2009
  • Habari Zinazolingana
  • Maagizo kwa Ndugu Walio na Migawo Katika Mkutano wa Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Mkutano wa Utumishi Hutuandalia Vifaa Kwa Ajili ya Kila Kazi Njema
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Unaalikwa kwa Uchangamfu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Mikutano ya Utumishi wa Shambani Inayotimiza Kusudi Lake
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2009
km 5/09 uku. 2

Jinsi ya Kutayarisha Mkutano wa Utumishi

1. Mkutano wa Utumishi unatusaidiaje, na tutanufaika hasa tukifanya nini?

1 Mkutano wa Utumishi umekusudiwa kutusaidia kuwa na matokeo mazuri katika huduma. Mambo makuu yanayozungumziwa ni kazi ya kuhubiri habari njema ya Ufalme, kufanya wanafunzi, na kutangaza hukumu ya Mungu inayokaribia. (Mt. 28:19, 20; Marko 13:10; 2 Pet. 3:7) Tunanufaika hasa na mkutano huu muhimu tunapotayarisha vizuri na kuwa tayari kutoa maelezo.

2. Tunaweza kujitayarisha jinsi gani kusikiliza hotuba itakayotolewa?

2 Hotuba: Mara nyingi, chanzo cha habari zitakazozungumziwa huonyeshwa katika maagizo kwa msemaji. Unaweza kupitia habari hizo, kusoma maandiko yasiyonukuliwa, na kutafakari kuhusu jinsi unavyoweza kuzitumia katika huduma yako.

3. Tunaweza kujitayarishaje kutoa maelezo wakati wa mazungumzo kwa maswali na majibu?

3 Mazungumzo kwa Maswali na Majibu: Sehemu hii itashughulikiwa kama Funzo la Mnara wa Mlinzi. Msemaji atatoa utangulizi na umalizio mfupi. Piga mstari chini ya mambo makuu katika kila fungu ili uwe tayari kutoa maelezo mafupi yanayokazia mambo ambayo yanazungumziwa.

4. Tunajitayarishaje kushiriki katika mazungumzo pamoja na wasikilizaji?

4 Mazungumzo Pamoja na Wasikilizaji: Sehemu hii ni hotuba, lakini mara kwa mara msemaji atawaomba wasikilizaji watoe maelezo. Ukipiga mstari chini ya mambo makuu na kusoma maandiko yasiyonukuliwa, huenda ukaweza kutoa maelezo maswali yanapoulizwa. Ndugu anayegawiwa sehemu hii atajitahidi kadiri iwezekanavyo kuwashirikisha wasikilizaji kutoa maelezo kuhusu mambo makuu.

5. Tunaweza kufanya nini ili tunufaike kabisa na maonyesho?

5 Maonyesho: Baadhi ya sehemu zina maonyesho kuhusu jinsi habari zinazozungumziwa zinavyoweza kutumiwa katika eneo lenu. Wazee, wahubiri wakomavu, au mapainia wataombwa kufanya maonyesho. Unaweza kujitayarisha kwa kujaribu kuwazia jinsi ndugu au dada watakavyoshughulikia maonyesho hayo. Wakati onyesho lililopendekezwa katika Huduma Yetu ya Ufalme linapotumiwa, fikiria jinsi ambavyo wewe ungesema kwa maneno yako, au jinsi unavyoweza kulibadili ili lifae wenye nyumba mbalimbali. Kumbuka kubeba kitabu au gazeti litakalotumiwa katika onyesho. Mnaweza kunufaika kwa kufanya maonyesho hayo wakati wa Ibada ya Familia.

6. Kuna sababu gani muhimu za kutayarisha Mkutano wa Utumishi?

6 Tutafurahia Mkutano wa Utumishi zaidi ikiwa tumejitayarisha vizuri na kufikiria mapema habari zitakazozungumziwa. Tukifuata mapendekezo ambayo tumepata tutatiana moyo hata zaidi. (Rom. 1:11, 12) Tutatimiza utume wetu kwa njia bora tukitenga wakati ili kutayarisha Mkutano wa Utumishi.—2 Tim. 3:17.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki