Je, Umewahi Kuanzisha Funzo Katika Ziara ya Kwanza?
Tunapowaeleza wenye nyumba kuhusu mpango wa kujifunza Biblia, baadhi yao wanasema hawana haja na funzo au wanajifunza Biblia kanisani. Kwa kuwa hawajui kwamba sisi tunajifunza Biblia kwa njia tofauti sana na vikundi vingine vya dini, hawawezi kuwazia jinsi ambavyo wangefurahia kujifunza Biblia pamoja nasi na kuielewa vizuri. Kwa hiyo, badala ya kueleza tu kuhusu funzo la Biblia, tumia dakika chache katika ziara ya kwanza kuonyesha jinsi ya kujifunza Biblia, yaani, usiwaambie tu wewe ni mpishi bora na kwamba utawaletea mlo waonje; acha waonje mara moja! Ona jinsi unavyoweza kuanzisha funzo kwa kutumia dakika chache tu, ukitumia pendekezo moja kwenye ukurasa wa 6 wa Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2006.
“Je, unafikiri maneno haya yatakuja kutimizwa? [Soma Isaya 33:24, kisha umruhusu ajibu.] Hebu nikuonyeshe jambo lenye kupendeza kuhusu habari hii.” Mpe mwenye nyumba kitabu Biblia Inafundisha, na umwombe afungue ukurasa wa 36, fungu la 22. Soma swali lililo chini kwenye ukurasa huu, kisha umwombe ajaribu kupata jibu huku ukisoma fungu hilo. Kisha uliza swali tena, na umsikilize mwenye nyumba anapojibu. Someni andiko lingine katika fungu hilo. Taja swali ambalo litajibiwa wakati ujao, na ufanye mpango hususa wa kurudi. Kuanzisha funzo ni rahisi hivyo!