Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Kuonyesha Jinsi Funzo la Biblia Linavyofanywa Kwa Kutumia Kitabu Biblia Inafundisha
Kwa Nini Ni Muhimu: Huenda watu wengi wasielewe tunachomaanisha tunaposema kwamba tunajifunza na watu Biblia bila malipo. Wanaweza kufikiri kwamba wanapaswa kujiunga na kikundi fulani cha kujifunza au kujifunza kupitia barua. Badala ya kumwambia tu tungependa kujifunza naye, kwa nini usimwonyeshe jinsi funzo linavyofanywa? Kwa dakika chache tu hata ikiwa ni mlangoni, unaweza kumwonyesha mtu jinsi kujifunza Biblia ni jambo rahisi na lenye manufaa.
Jaribu Dokezo Hili kwa Mwezi Mzima:
Sali kwa Yehova abariki jitihada zako za kuanzisha funzo la Biblia.—Flp. 2:13.
Jaribu kuonyesha jinsi funzo la Biblia linavyofanywa kwa kutumia kitabu Biblia Inafundisha, au onyesha video yenye kichwa Ni Nini Hutendeka Katika Funzo la Biblia? angalau mara moja unapokuwa katika huduma.