Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Juni 1
“Watu wengi hufanya uaguzi kwa kutazama nyota kabla ya kufanya maamuzi. Je, unafikiri maisha yetu yanaongozwa na nyota? [Mruhusu ajibu.] Ona kwamba Biblia inataja makundi-nyota ya unajimu. [Soma 2 Wafalme 23:5.] Makala hii inatoa maoni ya Biblia kuhusu jambo hilo.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 18.
Amkeni! Juni
“Mara nyingi makanisa hutoza malipo kwa ajili ya huduma kama vile ubatizo, arusi, na mazishi. Je, unafikiri inafaa kufanya hivyo? [Mruhusu ajibu.] Ona maagizo haya ambayo Yesu aliwapa wanafunzi wake. [Soma Mathayo 10:7, 8b.] Makala hii inaonyesha yale ambayo Biblia inasema kuhusu kutoza malipo kwa ajili ya huduma za kidini.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 22.
Mnara wa Mlinzi Julai 1
“Watu wengi husema kuwa jina la Mweza Yote ni Mungu. Hata hivyo, je, unajua kwamba Biblia inatujulisha jina la Mungu? [Mruhusu ajibu, kisha usome Isaya 42:8a.] Gazeti hili linaeleza kwa nini jina la Mungu limeondolewa katika Biblia fulani na umuhimu wa kumjua Mungu kwa jina.”
Amkeni! Julai
“Hali ya uchumi leo imewatia watu wasiwasi mwingi. Wale wasio na kazi wanafadhaika, ilhali wale walioajiriwa wana wasiwasi kuhusu kupoteza kazi zao. Je, unafikiri hili ni shauri zuri la kutusaidia kukabiliana na hali hizo? [Soma Mathayo 6:34, kisha umruhusu ajibu.] Gazeti hili linatoa mapendekezo kuhusu matumizi ya pesa na jinsi ya kushughulika na hisia zetu.”