Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Oktoba 1
“Watu wengi hujiuliza kama Mungu anajali tunapokumbwa na mahangaiko na huzuni. Wewe unaonaje? [Mruhusu ajibu, kisha usome Zaburi 34:18.] Makala inayoanzia ukurasa wa 19 inaonyesha jinsi Mungu hutusaidia kushinda hisia zisizofaa kama vile kujihisi kuwa hatufai, kuwa na huzuni nyingi, na kuhisi kuwa tuna hatia sana.”
Amkeni! Oktoba
“Watu fulani humwona Mungu kama nguvu fulani isiyo na utu. Wengine humwona kuwa mtu mwenye hisia. Una maoni gani? [Mruhusu ajibu.] Ona maneno haya yenye kupendeza. [Soma 1 Petro 5:6, 7.] Makala inayoanzia ukurasa wa 29 inatoa jibu la Biblia la swali hili: Je, Mungu Ni Mtu Halisi?”
Mnara wa Mlinzi Novemba 1
“Sisi sote tunatamani kuwa na uradhi. Unafikiri tunahitaji pesa ili tuwe na uradhi? [Mruhusu ajibu.] Mwandikaji mmoja wa Biblia alijifunza kuridhika alipokuwa na vitu vichache tu. [Soma Wafilipi 4:11, 12.] Gazeti hili linaonyesha njia tano za kupata uradhi, zinazopatikana katika Biblia.”
Amkeni! Novemba
“Baadhi ya watu wasioamini kwamba kuna Mungu wanaona kwamba ulimwengu ungekuwa bora zaidi bila dini kwa sababu mambo mengi mabaya yamefanywa kwa jina la Mungu. Wewe unaonaje? [Mruhusu ajibu.] Ona sababu moja inayofanya dini isababishe kuteseka kwa wanadamu. [Soma 2 Timotheo 4:3, 4.] Gazeti hili linaonyesha baadhi ya dhana zenye kasoro za watu wasioamini kwamba kuna Mungu.”