Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Oktoba 1
“Leo watu hawaamini kuna Muumba. Unafikiri ni kwa nini? [Mruhusu ajibu.] Andiko hili linatoa sababu moja. [Soma Habakuki 1:2, 3.] Makala hii inazungumzia mambo kadhaa kumhusu Mungu ambayo yamefanya watu wasimwamini.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 11.
Amkeni! Oktoba
“Je, unakubaliana nami kwamba familia zinakabili matatizo mengi leo? [Mruhusu ajibu.] Watu wengi hawajui kwamba Biblia ina mashauri mazuri sana. Kwa mfano, ona andiko hili. [Soma andiko moja katika gazeti.] Toleo hili la pekee la Amkeni! linaonyesha jinsi kanuni za Biblia zinavyoweza kuzisaidia familia zishughulikie ifaavyo hali mbalimbali.”
Mnara wa Mlinzi Novemba 1
“Je, unafikiri kwamba mambo yote yanayofundishwa makanisani yanatoka katika Biblia? [Mruhusu ajibu.] Biblia inatuonya kuwa waangalifu ili tusidanganyike. [Soma Wakolosai 2:8.] Gazeti hili linafichua mambo sita yasiyopatana na Neno la Mungu ambayo yamefundishwa kwa muda mrefu.”
Amkeni! Novemba
“Vifaa kama simu ya mkononi na kompyuta ni vitu vya kawaida siku hizi. Je, unafikiri vitu hivyo vinaokoa au vinapoteza wakati? [Mruhusu ajibu.] Yaelekea watu wengi wangekubali kwamba inafaa kufuata shauri hili kuhusu kutumia wakati kwa hekima. [Soma Waefeso 5:15, 16.] Gazeti hili linaonyesha jinsi tunavyoweza kutumia vifaa hivyo kwa usawaziko na kwa kuwafikiria wengine.”