“Upendeni Ushirika Mzima wa Akina Ndugu”
Maneno yaliyoongozwa na roho ya kichwa hicho yaliandikwa karibu miaka elfu mbili hivi iliyopita. (1 Pet. 2:17) Lakini, tunahitaji kuyatumia maneno hayo sasa kuliko wakati mwingine wowote! Tunawezaje kuupenda undugu wa ulimwenguni pote ulioenea hivyo? Na katika ulimwengu huu usio na upendo, tunawezaje kuhakikisha kwamba upendo wetu haufifii? (Mt. 24:12) Ona ikiwa unaweza kujibu maswali yafuatayo unapotazama video Our Whole Association of Brothers.
(1) Ni wakati gani tulikuja kuwa rasmi sehemu ya undugu wa Kikristo? (2) Ni mambo gani matatu ambayo sisi hushiriki pamoja na ndugu zetu ulimwenguni pote? (3) Ndugu zetu wanaonyeshaje azimio lao la kuhubiri (a) katika nyika ya Alaska, (b) katika bandari kubwa za Ulaya, na (c) katika misitu minene ya Peru? (4) Kwa nini kazi yetu ya kuhubiri ni ya pekee sana? (5) Toa mifano inayoonyesha jinsi Mashahidi wa Yehova wamefarijiana na kutegemezana (a) baada ya tetemeko la ardhi, (b) baada ya kimbunga, na (c) wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe? (6) Ni kwa njia zipi sisi sote tunaweza kuonyesha alama kuu ya undugu wetu wa Kikristo? (Yoh. 13:35) (7) Kuna faida gani za kufanya kazi pamoja tunapojenga Majumba yetu ya Ufalme? (8) Ndugu zetu katika Ulaya Mashariki na Urusi waliwezaje kubaki imara kiroho wakati kazi yetu ilipopigwa marufuku? (9) Mashahidi wengi hufanya jitihada gani za pekee ili kuhudhuria makusanyiko, na kwa nini? (10) Video hii imeimarishaje azimio lako (a) la kumwabudu Yehova kwa umoja pamoja na ndugu zako katika mikutano ya Kikristo, (b) la kuwasaidia wengine wakati wa hali ngumu, na (c) la kuhubiri kwa uaminifu wakati wowote na kwa njia yoyote uwezayo? (11) Ni jinsi gani na wakati gani tunaweza kutumia video hii katika utumishi?
Sababu yetu kuu ya kuwa sehemu ya undugu wetu wa Kikristo ni upendo wetu kwa Yehova. Kwa hiyo, tunapenda kujifunza habari zake na kuwafundisha wengine kumhusu. Na tunawapenda watu ambao Yehova anawapenda. Tunapowasaidia wakati wanapokabili hali ngumu, hatutazamii Mungu atushukuru kwa kufanya hivyo. Badala yake, tunamshukuru Mungu kwa sababu tunaona undugu wetu wa Kikristo kuwa zawadi yenye thamani kutoka kwake. Kadiri siku za mwisho za ulimwengu huu usio na upendo zinavyokaribia kikomo, na tuendelee kuupenda ushirika mzima wa akina ndugu!