Trakti Habari za Ufalme Na. 38 Itagawanywa Mwezi wa Novemba!
1. Watu hujiuliza nini kuhusu wafu, na maswali hayo yatajibiwaje mwezi wa Novemba?
1 Hata iwe watu wanaamini nini, kifo ni adui ya watu wote. (1 Kor. 15:26) Watu wengi hawajui wafu wako wapi na wanajiuliza ikiwa wataweza kuwaona tena. Kwa hiyo, makutaniko ulimwenguni pote yatashiriki katika kampeni ya mwezi mzima ya kugawanya trakti Habari za Ufalme Na. 38 yenye kichwa “Je, Kweli Wafu Wataishi Tena?” Kampeni hiyo ya pekee itaanza tarehe 1 mwezi wa Novemba. Baada ya kampeni, trakti hiyo itakuwa ikitumiwa katika huduma ya shambani kama trakti nyinginezo.
1. Watu hujiuliza nini kuhusu wafu, na maswali hayo yatajibiwaje mwezi wa Novemba?
2. Eleza jinsi trakti Habari za Ufalme Na. 38 ilivyo.
2 Jinsi Ilivyo: Trakti Habari za Ufalme Na. 38 inaweza kukunjwa ili sehemu ya mbele ionyeshe kichwa chake chenye kusisimua pamoja na maneno “Ungejibuje swali hilo . . . ndiyo? hapana? labda?” Msomaji anapoifungua anaweza kupata majibu ya Biblia ya kichwa cha trakti hiyo ambacho ni swali, na pia jinsi anavyoweza kunufaika na ahadi za Biblia. Pia ataona sababu zinazoweza kumsadikisha aiamini Biblia. Sehemu ya nyuma ya trakti hiyo ina swali zuri ambalo msomaji anaweza kulifikiria na kumfanya ajifunze mengi zaidi.
3. Trakti Habari za Ufalme Na. 38 itagawanywa vipi?
3 Jinsi Itakavyogawanywa: Kampeni hii haina tofauti yoyote na ile ya kugawanya mialiko ya Ukumbusho na mialiko ya kusanyiko la wilaya. Wazee watatoa mwongozo kuhusu jinsi eneo litakavyohubiriwa kama ilivyotajwa katika barua waliyopokea ya Aprili 1, 2013. Makutaniko yaliyo na eneo dogo la kuhubiri yanaweza kujitolea kuyasaidia makutaniko yenye maeneo makubwa. Unapochukua trakti Habari za Ufalme Na. 38, kumbuka kuchukua tu kiasi utakachohitaji kwa juma moja. Wakati wa kampeni hiyo, mnaweza kugawanya trakti hiyo mnapohubiri hadharani baada ya kumaliza kuhubiri nyumba zote katika eneo lenu. Mkimaliza kugawanya trakti zote kabla ya mwisho wa mwezi, mnaweza kuhubiri kwa kutumia machapisho yanayotolewa mwezi huo. Katika Jumamosi ya kwanza ya mwezi huo wa Novemba, tutakazia fikira kugawanya trakti hiyo badala ya kuanzisha mafunzo ya Biblia. Hali zinaporuhusu, tutatoa magazeti Jumamosi na Jumapili. Je, unafanya mipango ili ushiriki kikamilifu katika kampeni hiyo ya pekee?