Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/14 uku. 2
  • Usiwe Mwandamani Anayenyamaza Tu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Usiwe Mwandamani Anayenyamaza Tu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Habari Zinazolingana
  • Msaidie Mwenzako Mlangoni
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Kujengana Tunapokuwa Katika Huduma
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Kusaidia Wengine Tunapokuwa Katika Utumishi wa Shambani
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Dumisha Bidii Yako Katika Huduma
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2014
km 1/14 uku. 2

Usiwe Mwandamani Anayenyamaza Tu

1. Tunaweza kuigaje mtazamo wa Paulo tunapokuwa utumishi na wahubiri wengine?

1 Mtume Paulo aliuona muda aliotumia pamoja na waamini wenzake kuwa fursa nzuri za ‘kubadilishana kitia-moyo.’ (Rom. 1:12) Unapokuwa na mhubiri mwingine katika utumishi wa shambani, je, unatumia muda huo kumsaidia na kumtia moyo? Badala ya kuwa mwandamani anayenyamaza tu, kwa nini usishiriki naye mambo ambayo yamekusaidia kuwa mhubiri mwenye matokeo?

2. Tunaweza kufanyaje ili kumpa ujasiri mwandamani wetu, na kwa nini hilo ni muhimu?

2 Mpe Ujasiri: Wahubiri wengine wanakosa ujasiri, jambo ambalo huenda likaonekana kupitia ishara za mwili na sauti zao. Tunaweza kuongeza ujasiri wao kwa kuwapongeza kutoka moyoni. Kuna njia gani nyingine za kuwaongezea ujasiri? Mwangalizi mmoja anayesafiri humwambia mwandamani wake kwa uhuru jinsi yeye mwenyewe anavyoogopa na vile ambavyo husali mara nyingi ili apate msaada wa kukabiliana na hali hiyo. Ndugu mwingine alisema hivi kuhusu kilichomsaidia kuwa na ujasiri: “Anza kwa tabasamu. Wakati mwingine ninahitaji kusali ili nipate msaada wa kufanya tu jambo hilo dogo.” Je, kuna jambo ambalo limekusaidia kuwa na ujasiri unapokuwa katika utumishi wa shambani? Zungumzieni jambo hilo na mwandamani wako.

3. Tunaweza kushiriki jambo gani na mwandamani wetu ambalo litamsaidia kuwa na matokeo zaidi katika huduma?

3 Shiriki Naye Mbinu za Kuhubiri: Je, umepata utangulizi rahisi au swali, labda jambo linalohusu tukio fulani katika eneo lenu, linaloweza kuwa na matokeo kuanzisha mazungumzo? Licha ya mapendekezo tunayopokea kwa ajili ya utumishi, je, umepata matokeo mazuri kwa kutumia maneno yako mwenyewe katika utangulizi wako? Mwambie mwandamani wako. (Met.  27:17) Mnapoenda kwenye ziara ya kurudia, unaweza kumwambia kusudi la ziara hiyo na jinsi ya kutimiza kusudi hilo. Baada ya funzo la Biblia, unaweza kumweleza kwa nini ulichagua jambo fulani kuu, andiko, au mbinu ili kuzungumzia mahitaji ya mwanafunzi.

4. Kwa nini tupendezwe kuwasaidia wahubiri wenzetu?

4 Waeneza-injili wa karne ya kwanza walifanya mengi zaidi ya kuwasaidia wasioamini. Walitambua pia umuhimu wa kutiana moyo na kutiana nguvu. (Mdo. 11:23; 15:32) Mtume Paulo alimzoeza kijana Timotheo na kisha akamtia moyo awaeleze wengine mambo aliyokuwa amejifunza. (2 Tim. 2:2) Tunapokumbuka kuwafanyia mema Wakristo wenzetu tunapokuwa katika huduma, tunaongeza shangwe yao na kuwasaidia waweze kuwa na matokeo zaidi katika utumishi na jambo la muhimu hata zaidi tunampendeza Baba yetu wa mbinguni.—Ebr. 13:15, 16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki