Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/14 uku. 2
  • Wachukueni Manabii Kuwa Kielelezo—Nahumu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wachukueni Manabii Kuwa Kielelezo—Nahumu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Habari Zinazolingana
  • Kitabu cha Biblia Namba 34—Nahumu
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Nahumu, cha Habakuki, na cha Sefania
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Wokovu Unawezekana Mungu Alipizapo Kisasi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Nahumu—Yaliyomo
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2014
km 9/14 uku. 2

Wachukueni Manabii Kuwa Kielelezo—Nahumu

1. Tunajifunza nini katika kitabu cha Nahumu?

1 Magofu ya jiji la kale la Ninawi yanathibitisha kwamba, kama tu Nahumu alivyotoa unabii, Yehova anawalipiza kisasi adui Zake, na hata mpinzani mkatili sana hawezi kusimama dhidi Yake. (Nah. 1:2, 6) Tunajifunza mambo mengi tunayoweza kutumia katika utumishi wetu kwa kuchunguza kwa makini unabii wa Nahumu.

2. Tunawezaje kufanya ujumbe wetu uwe wenye kutia moyo?

2 Toa Faraja na Tumaini: Huenda, kitabu cha Nahumu kinaonekana tu kuwa tangazo la uharibifu wa Ninawi, jiji kuu la Ashuru ya kale. (Nah. 1:1; 3:7) Hata hivyo, tangazo hilo lilikuwa habari njema kwa watu wa Yehova. Nahumu, ambaye jina lake linamaanisha “Mfariji,” aliwahakikishia Wayahudi wenzake kwamba adui zao wangeangamizwa karibuni! Zaidi ya hayo, aliwahakikishia kwamba Yehova “ni ngome katika siku ya taabu.” (Nah. 1:7) Sisi pia, tunawahubiria watu habari njema na kuwatia moyo watafute kimbilio katika Yehova.—Nah. 1:15.

3. Ni katika njia gani tunaweza kumwiga Nahumu katika kutumia mifano au vielelezo?

3 Tumia Mifano na Vielelezo: Yehova alimwongoza Nahumu kulinganisha uharibifu wa Ninawi na ule wa jiji la Thebes (No-amoni) huko Misri, ambalo awali liliharibiwa na Ashuru. (Nah. 3:8-10) Tunapowaambia watu kuhusu mwisho wa mfumo huu mwovu wa mambo, tunaweza kufafanua unabii wa Biblia unaothibitisha kwamba Yehova hutimiza kila jambo analoahidi. Kwa mfano, Wababiloni na Wamedi walipokuwa wakivamia jiji la Ninawi mwaka wa 632 K.W.K., mvua kubwa zilisababisha mafuriko katika Mto Tigri na hivyo kubomoa sehemu ya kuta imara za jiji hilo. Kwa hiyo, jiji la Ninawi likatekwa kwa urahisi kama tu Yehova alivyotabiri.—Nah. 1:8; 2:6.

4. Tunawezaje kusema kwa njia iliyo wazi na inayoeleweka katika huduma?

4 Sema kwa Njia Iliyo Wazi na Inayoeleweka: Nahumu aliandika kwa njia iliyo wazi na yenye kusisimua. Ujumbe wake ulieleweka. (Nah. 1:14; 3:1) Vivyo hivyo, tungependa kutumia lugha inayoeleweka kwa urahisi. (1 Kor. 14:9) Katika ziara ya kwanza, mweleze mtu waziwazi kusudi la kumtembelea. Unapowafundisha wengine Biblia, wasaidie wasitawishe imani kumwelekea Yehova na Neno lake na waone jinsi habari wanayojifunza inavyowahusu wao binafsi.—Rom. 10:14.

5. Tunapata uhakikisho gani katika unabii wa Nahumu?

5 Kitabu cha Nahumu kinaonyesha waziwazi jinsi nabii huyo alivyotumaini utimizo hakika wa neno la Yehova. Tunapokaribia mwisho wa mfumo wa Shetani, tunafarijiwa sana na maneno haya ya Mungu: “Taabu haitazuka mara ya pili.”—Nah. 1:9.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki