Kwa Nini Tuwe na “Bidii kwa Ajili ya Kazi Njema?”
Je, una bidii kwa ajili ya kazi njema? Tukiwa wahubiri wa Ufalme, tuna kila sababu ya kuwa na bidii. Kwa nini? Fikiria yale tunayosoma katika Tito 2:11-14:
Mstari wa 11: “Fadhili zisizostahiliwa za Mungu” ni nini, nasi tumefaidika jinsi gani kutokana nazo?—Rom. 3:23, 24.
Mstari wa 12: Tumefaidika jinsi gani kutokana na fadhili zisizostahiliwa za Mungu?
Mstari wa 13 na 14: Kwa kuwa tumesafishwa, tuna tumaini gani la wakati ujao? Tumesafishwa kutokana na mwenendo wa ulimwengu wa kutomwogopa Mungu kwa kusudi gani kuu?
Mistari hiyo inakuchocheaje kuwa na bidii kwa ajili ya kazi njema?