Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Mnara wa Mlinzi Desemba 1
“Tumekutembelea kifupi ili kurekebisha maoni yasiyofaa ya watu wengi kuhusu Biblia. Watu wengi wanaiheshimu Biblia, lakini wanahisi ni vigumu sana kuielewa. Wewe una maoni gani kuhusu Biblia? [Mruhusu ajibu.] Ona sababu moja inayotuchochea tuwe na hamu ya kuielewa Biblia. [Soma Waroma 15:4.] Gazeti hili linaeleza kwa nini tuna uhakika kwamba Biblia iliandikwa ili tuielewe. Pia, lina madokezo ya kutusaidia kuielewa.”
Amkeni! Desemba
“Tumewatembelea kwa muda mfupi tukiwa na ujumbe kwa ajili ya familia. Kila mtu hupenda nyumbani kuwe na amani na umoja. Unafikiri ni nini kinachofaa zaidi—kujitahidi kuepuka kutofautiana katika familia au kujifunza jinsi ya kutatua hali hiyo? [Mruhusu ajibu.] Ona methali hii ya Biblia. [Soma Methali 26:20.] Gazeti hili linaonyesha ushauri ambao Biblia inawapa watu wa familia ili wawe na amani zaidi.”