HAZINA ZA NENO LA MUNGU | ISAYA 24-28
Yehova Huwatunza Watu Wake
Kama mkaribishaji mkarimu, Yehova anatuandalia chakula kingi cha kiroho.
“Yehova wa majeshi hakika atavifanyia vikundi vyote vya watu . . . karamu”
Katika nyakati za Biblia, watu walipokula mlo pamoja walionyesha kwamba kuna amani na urafiki kati yao
“Ya vyakula vinono vilivyotiwa mafuta vilivyojazwa urojorojo, ya divai iliyowekwa kwenye machicha, iliyochujwa”
Vyakula vinono na divai iliyowekwa kwenye machicha, iliyochujwa inawakilisha chakula bora kabisa cha kiroho ambacho Yehova anatuandalia