HAZINA ZA NENO LA MUNGU | MATHAYO 1-3
“Ufalme wa Mbinguni Umekaribia”
Kutokana na jinsi Yohana alivyovalia na kuonekana, mtu angeweza kutambua mara moja kwamba aliishi maisha rahisi na alijitoa kikamili kufanya mapenzi ya Mungu
Mambo yote ambayo Yohana alijidhabihu hayawezi kulinganishwa na pendeleo la pekee ambalo alipata la kuwa mtayarishaji wa njia wa Yesu
Maisha rahisi yanatusaidia kufanya mengi katika utumishi wa Mungu na hivyo tunaridhika sana. Tunaweza kurahisisha maisha yetu kwa . . .
kutambua vitu tunavyohitaji hasa
kupunguza gharama zisizo za lazima
kutayarisha bajeti inayofaa mahitaji yetu
kutupa au kugawa vitu tusivyotumia
kulipa madeni yote
kutotumia muda mwingi kupita kiasi katika kazi ya kimwili
Chakula cha Yohana kilikuwa nzige na asali ya mwituni
Maisha rahisi yatanisaidia kufuatilia mradi gani?