Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb18 Mei uku. 8
  • “Kile Ambacho Mungu Ameunganisha . . . ”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Kile Ambacho Mungu Ameunganisha . . . ”
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2018
  • Habari Zinazolingana
  • Talaka Biblia Inasema Nini Hasa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Heshimu “Kile Ambacho Mungu Ameunganisha”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • Kujitahidi Kufanya Maendeleo Katika Ndoa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Talaka Huwa na Majeruhi
    Amkeni!—1991
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2018
mwb18 Mei uku. 8
Mwanamume na mwanamke wakishikana mkono

MAISHA YA MRISTO

“Kile Ambacho Mungu Ameunganisha . . . ”

Sheria ya Musa ilisema kwamba mwanamume aliyetaka kutoa talaka alipaswa kutayarisha hati ya kisheria. Hilo liliwazuia watu wasivunje ndoa zao ovyoovyo. Hata hivyo, katika siku za Yesu, viongozi wa kidini walifanya iwe rahisi kutoa talaka. Wanaume wangeweza kuwataliki wake zao kwa sababu yoyote ile. (“cheti cha kumfukuza” habari za utafiti Mk 10:4, nwtsty; “anayetaliki mke wake,” “anafanya uzinzi dhidi yake” habari za utafiti Mk 10:11, nwtsty) Yesu aliwakumbusha kwamba Yehova ndiye aliyeidhinisha na kuanzisha mpango wa ndoa. (Mk 10:2-12) Mume na mke walipaswa kuwa “mwili mmoja” katika muungano wa kudumu. Msingi pekee wa talaka kulingana na simulizi la Mathayo, ni “uasherati.”—Mt 19:9.

Leo, watu wengi wana maoni kama ya Mafarisayo kuhusu ndoa, si kama ya Yesu. Matatizo yanapozuka, watu ulimwenguni hutoa talaka bila kukawia. Kwa upande mwingine, wenzi wa ndoa Wakristo, wanachukua kwa uzito viapo vyao vya ndoa na wanajitahidi kukabiliana na matatizo kwa kutumia kanuni za Biblia. Tazameni video Upendo na Heshima Hufanya Familia Ziwe na Umoja, kisha mjibu maswali yafuatayo:

  • Kusoma Biblia; mume akimsikiliza mke wake anapojieleza; picha ya harusi iliyoraruliwa

    Unaweza kutumiaje Methali 15:1 katika ndoa yako, na kwa nini kanuni hiyo ni muhimu?

  • Unaweza kuepukaje matatizo kwa kutumia Methali 19:11?

  • Ikiwa ndoa yako iko katika hali mbaya, badala ya kuanza kujiuliza ikiwa utafute talaka, unapaswa kujiuliza maswali gani?

  • Unawezaje kuwa mume au mke bora kwa kutumia andiko la Mathayo 7:12?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki