HAZINA ZA NENO LA MUNGU | KUTOKA 8-9
Farao Mwenye Kiburi Atumiwa Kutimiza Kusudi la Mungu
Mafarao wa Misri walijiona kuwa miungu. Hilo linatusaidia kuelewa sababu iliyomfanya Farao awe na kiburi sana hivi kwamba akakataa kumsikiliza Musa na Haruni na hata makuhani wake wachawi.
Je, wewe husikiliza mapendekezo yanayotolewa na watu wengine? Je, unathamini unaposhauriwa? Au je, wewe huhisi kwamba sikuzote uko sahihi? “Kiburi hutangulia kuanguka kwa kishindo.” (Met 16:18) Ni muhimu sana kuepuka kuwa na kiburi.