MAISHA YA MKRISTO
Simama Imara Mwisho Unapozidi Kukaribia
KWA NINI NI MUHIMU?: Hivi karibuni matukio yenye kustaajabisha yatatokea na tutahitaji kuwa jasiri na kumtegemea Yehova kuliko wakati mwingine wowote. Dhiki kuu itaanza kwa kuharibiwa kwa dini ya uwongo. (Mt 24:21; Ufu 17:16, 17) Katika kipindi hicho chenye msukosuko, tutahitaji kuhubiri ujumbe wa hukumu. (Ufu 16:21) Tutakabili shambulizi kutoka kwa Gogu wa Magogu. (Eze 38:10-12, 14-16) Kisha Yehova atawalinda watu wake kwa kuleta “vita vya siku kuu ya Mungu Mweza-Yote.” (Ufu 16:14, 16) Ili tuweze kukabiliana na matukio hayo ya wakati ujao kwa ujasiri, tunahitaji kuendelea kudumisha ushikamanifu wetu imani yetu inapojaribiwa sasa.
JINSI YA KUFANYA HIVYO:
Tetea kwa ujasiri viwango vya juu vya maadili vya Yehova.—Isa 5:20
Endelea kuabudu pamoja na Wakristo wenzako.—Ebr 10:24, 25
Fuata haraka mwongozo kutoka kwa tengenezo la Yehova.—Ebr 13:17
Tafakari kuhusu jinsi Yehova alivyowaokoa watu wake nyakati za kale.—2Pe 2:9
Sali kwa Yehova, na umtegemee.—Zb 112:7, 8
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA MATUKIO YA WAKATI UJAO YATAKAYOHITAJI UJASIRI—KISEHEMU, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Utii wa wahubiri ulijaribiwaje kutaniko lao lilipounganishwa na makutaniko mengine?
Kuna uhusiano gani kati ya ujasiri na utii?
Kwa nini tutahitaji ujasiri Har–Magedoni itakapokuja?
Jitayarishe sasa kukabiliana na matukio ya wakati ujao yatakayojaribu ujasiri wetu
Ni simulizi gani la Biblia linaloweza kutusaidia kuimarisha imani yetu katika nguvu za Yehova za kuokoa?—2Nya 20:1-24