Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb20 Agosti uku. 3
  • Simama Imara Mwisho Unapozidi Kukaribia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Simama Imara Mwisho Unapozidi Kukaribia
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2020
  • Habari Zinazolingana
  • Sitawisha Sifa Zinazompendeza Mungu​—Ujasiri
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2017
  • Kuwa Jasiri Si Vigumu Sana
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2021
  • “Uwe Hodari . . . Nawe Utende”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Nipe Ujasiri
    ‘Mwimbieni Yehova kwa Shangwe’
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2020
mwb20 Agosti uku. 3

MAISHA YA MKRISTO

Simama Imara Mwisho Unapozidi Kukaribia

KWA NINI NI MUHIMU?: Hivi karibuni matukio yenye kustaajabisha yatatokea na tutahitaji kuwa jasiri na kumtegemea Yehova kuliko wakati mwingine wowote. Dhiki kuu itaanza kwa kuharibiwa kwa dini ya uwongo. (Mt 24:21; Ufu 17:16, 17) Katika kipindi hicho chenye msukosuko, tutahitaji kuhubiri ujumbe wa hukumu. (Ufu 16:21) Tutakabili shambulizi kutoka kwa Gogu wa Magogu. (Eze 38:10-12, 14-16) Kisha Yehova atawalinda watu wake kwa kuleta “vita vya siku kuu ya Mungu Mweza-Yote.” (Ufu 16:14, 16) Ili tuweze kukabiliana na matukio hayo ya wakati ujao kwa ujasiri, tunahitaji kuendelea kudumisha ushikamanifu wetu imani yetu inapojaribiwa sasa.

JINSI YA KUFANYA HIVYO:

  • Tetea kwa ujasiri viwango vya juu vya maadili vya Yehova.​—Isa 5:20

  • Endelea kuabudu pamoja na Wakristo wenzako.​—Ebr 10:24, 25

  • Fuata haraka mwongozo kutoka kwa tengenezo la Yehova.​—Ebr 13:17

  • Tafakari kuhusu jinsi Yehova alivyowaokoa watu wake nyakati za kale.​—2Pe 2:9

  • Sali kwa Yehova, na umtegemee.​—Zb 112:7, 8

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA MATUKIO YA WAKATI UJAO YATAKAYOHITAJI UJASIRI—KISEHEMU, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Picha kutoka kwenye video ‘Matukio ya Wakati Ujao Yatakayohitaji Ujasiri.’ Kwenye Jumba la Ufalme, dada mwenye anatazama kwa wasiwasi baada ya kusoma migawo ya jinsi makutaniko yatakavyounganishwa.

    Utii wa wahubiri ulijaribiwaje kutaniko lao lilipounganishwa na makutaniko mengine?

  • Picha kutoka kwenye video ‘Matukio ya Wakati Ujao Yatakayohitaji Ujasiri.’ Dada yuleyule akizungumza kuhusu migawo ya kutaniko jipya na dada wengine wawili.

    Kuna uhusiano gani kati ya ujasiri na utii?

  • Picha kutoka kwenye video ‘Matukio ya Wakati Ujao Yatakayohitaji Ujasiri.’ Mvulana akiwa na wasiwasi baada ya kutafakari picha ya Har–​Magedoni kwenye kitabu ‘Ufalme wa Mungu Unatawala!’

    Kwa nini tutahitaji ujasiri Har–Magedoni itakapokuja?

  • Picha kutoka kwenye video ‘Matukio ya Wakati Ujao Yatakayohitaji Ujasiri.’ Yehoshafati na wengine kutoka Yuda wakifika kwenye uwanja wa vita na kugundua kwamba hakuna askari aliyeachwa akiwa hai.

    Jitayarishe sasa kukabiliana na matukio ya wakati ujao yatakayojaribu ujasiri wetu

    Ni simulizi gani la Biblia linaloweza kutusaidia kuimarisha imani yetu katika nguvu za Yehova za kuokoa?​—2Nya 20:1-24

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki