HAZINA ZA NENO LA MUNGU | MAMBO YA WALAWI 4-5
Mpe Yehova Kilicho Bora
Umaskini haukumzuia mtu yeyote katika Israeli kufanya amani na Yehova. Hata maskini zaidi katika Israeli angeweza kumtolea Yehova dhabihu iliyokubalika, maadamu alitoa kilicho bora. Angeweza kutoa unga, lakini Yehova alitazamia uwe “laini,” ambao ulipewa wageni waheshimiwa. (Mwa 18:6) Leo, Yehova bado anatarajia tumpe kilicho bora. Hata ikiwa kile tunachompa ni kidogo sana, Yehova atakikubali ikiwa tumempa “dhabihu” yetu bora.—Ebr 13:15.
Kufahamu hilo kunaweza kukutiaje moyo ikiwa huwezi kufanya mengi kama zamani, labda kwa sababu ya kuzorota kwa afya au nguvu?