Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb20 Desemba uku. 3
  • Tunaonyesha Upendo kwa Kuunga Mkono Nidhamu Inayotoka kwa Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tunaonyesha Upendo kwa Kuunga Mkono Nidhamu Inayotoka kwa Yehova
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2020
  • Habari Zinazolingana
  • Nidhamu—Wonyesho wa Upendo wa Yehova
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2021
  • Nidhamu Inayoweza Kuzaa Tunda Lenye Kuamanika
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Kutenga na Ushirika Ni Mpango Wenye Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Mpendwa Wako Anapomwacha Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2020
mwb20 Desemba uku. 3

MAISHA YA MKRISTO

Tunaonyesha Upendo kwa Kuunga Mkono Nidhamu Inayotoka kwa Yehova

Kutenga na ushirika hulinda kutaniko na kuwatia nidhamu wakosaji wasiotubu. (1Ko 5:6, 11) Tunaonyesha upendo tunapounga mkono nidhamu hiyo kutoka kwa Yehova. Hilo linawezekanaje ikiwa kutenga na ushirika huwaumiza wote wanaohusika kutia ndani watu wa karibu wa ukoo na pia halmashauri ya hukumu?

Zaidi ya yote, upendo wetu unatuchochea kuhakikisha jina la Yehova linaendelea kuheshimiwa na viwango vyake vya utakatifu vinadumishwa. (1Pe 1:14-16) Pia tunaonyesha kwamba tunampenda yule aliyetengwa na ushirika. Nidhamu kama hiyo ingawa ni yenye kuumiza inaweza ‘kutokeza amani na uadilifu.’ (Ebr 12:5, 6, 11) Tunaposhirikiana na mtu aliyetengwa na ushirika au aliyejitenga, tunamzuia mtu huyo kufaidika na nidhamu ya Yehova. Kumbuka, Yehova huwatia nidhamu watu wake “kwa kiwango kinachofaa.” (Yer 30:11) Tunaendelea kutumaini kwamba mtu huyo atamrudia Baba yetu mwenye rehema. Kwa sasa tunaendelea kuunga mkono njia ya Yehova ya kutoa nidhamu na kufanya yote tunayoweza ili kudumisha uhusiano wetu pamoja na Yehova ukiwa imara.​—Isa 1:16-18; 55:7.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA DUMISHA USHIKAMANIFU UKIWA NA MOYO IMARA KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Picha kutoka kwenye video ‘Dumisha Ushikamanifu Ukiwa na Moyo Imara.’ Gabriella na Ben wakilia baada ya kusoma barua kutoka kwa mwana wao aliyeondoka nyumbani.

    Wazazi Wakristo huhisi maumivu kadiri gani mtoto wao anapomwacha Yehova?

  • Picha kutoka kwenye video ‘Dumisha Ushikamanifu Ukiwa na Moyo Imara.’ Marafiki wakiwakumbatia Gabriella na Ben baada ya mkutano wa kutaniko.

    Kutaniko linaweza kuwaungaje mkono washiriki wa familia ambao ni waaminifu?

  • Picha kutoka kwenye video ‘Dumisha Ushikamanifu Ukiwa na Moyo Imara.’ Gabriella akiwazia simulizi kuhusu uasi wa Kora.

    Ni simulizi gani la Biblia linaloonyesha kwamba kuwa mshikamanifu kwa Yehova ni muhimu kuliko kuwa mshikamanifu kwa watu wa familia?

  • Picha kutoka kwenye video ‘Dumisha Ushikamanifu Ukiwa na Moyo Imara.’ Baada ya mkutano, Gabriella anamwambia Ben kuhusu ujumbe wa simu kutoka kwa mwana wao.

    Tunaweza kuonyeshaje kwamba sisi ni washikamanifu kwa Yehova kuliko tulivyo washikamanifu kwa watu wa familia?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki