HAZINA ZA NENO LA MUNGU | MAMBO YA WALAWI 12-13
Jifunze Kutokana na Sheria Kuhusu Ukoma
Kanuni zinazofanyiza sheria kuhusu ukoma zinaweza kutufundisha nini kuhusu kulinda afya yetu ya kiroho?
Yehova aliwafundisha makuhani jinsi ya kutambua ukoma upesi. Wachungaji Wakristo leo wako tayari kutoa msaada upesi kwa yeyote anayehitaji msaada wa kiroho.—Yak 5:14, 15
Waisraeli walipaswa kuharibu kitu chochote kilichoambukizwa ukoma ili kuzuia ugonjwa usienee. Vivyo hivyo, Wakristo wanapaswa kuwa tayari kuacha kitu kilicho na thamani kwao, badala ya kukiruhusu kiwaongoze kutenda dhambi. (Mt 18:8, 9) Hilo linaweza kutia ndani mazoea, marafiki, au burudani
Mkristo anaweza kuonyeshaje kwamba anatamani sana kupata msaada wa Yehova?