Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yb05 kur. 3-5
  • Barua Kutoka Kwa Baraza Linaloongoza

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Barua Kutoka Kwa Baraza Linaloongoza
  • 2005 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Habari Zinazolingana
  • Matukio Muhimu Ya Mwaka Uliopita
    2005 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Matukio Muhimu ya Mwaka Uliopita
    2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Matukio Muhimu ya mwaka uliopita
    2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Barua Kutoka Kwa Baraza Linaloongoza
    2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
Pata Habari Zaidi
2005 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
yb05 kur. 3-5

Barua Kutoka Kwa Baraza Linaloongoza

TUNAPOKARIBIA ulimwengu mpya, ni muhimu kuendelea kumtarajia Yehova. (Sef. 3:8) Nabii Danieli alisema kwamba ‘Mungu ni Mfunuaji wa siri, naye amejulisha mambo yatakayotokea katika siku za mwisho.’ (Dan. 2:28) Ni pendeleo lililoje kuishi mwishoni mwa kipindi hiki kilichotabiriwa na kuelewa siri ambazo Yehova anafunua sasa!

Kupitia “mtumwa mwaminifu na mwenye busara,” Yehova amefunua hatua kwa hatua kusudi lake la kukusanya “umati mkubwa” wa waabudu katika ‘siku hizi za mwisho’ zenye taabu. (Mt. 24:45; Ufu. 7:9; 2 Tim. 3:1) Andiko la Isaya 2:2, 3 linasema kwamba umati huo ungekusanywa ulimwenguni pote “katika siku za mwisho.” Kukusanywa huko kunaendelea kila mwaka licha ya misukosuko na jeuri ambayo imeenea ulimwenguni.

Katika mwaka wa 2004, tulipata ufahamu zaidi kuhusu umuhimu wa kutii maneno haya ya Yesu: “Endeleeni kukesha . . . Iweni tayari.” (Mt. 24:42, 44) Kwa kweli mambo yanayotukia ulimwenguni leo yana maana kubwa kwa Wakristo wanaotambua “ishara za nyakati.” (Mt. 16:1-3) Ili atimize Neno lake, Yehova ataendelea kuwa na watu ambao amewapanga wafanye kazi yake licha ya upinzani ambao huenda ukawapata.

Ingawa wengine wanajitahidi kuzuia au kukomesha kazi ya kuhubiri kuhusu Ufalme, ndugu zetu wanaendelea kuhubiri kweli na kukutanika pamoja. (Mdo. 5:19, 20; Ebr. 10:24, 25) Mnamo Juni 2004 mahakama ya rufaa ya Moscow, nchini Urusi, iliunga mkono uamuzi uliotolewa na mahakama ya chini wa kupiga marufuku kazi ya Mashahidi wa Yehova na kufutilia mbali shirika lao jijini humo. Hata hivyo, ndugu hawakuvunjika moyo; wanajua yale ambayo Mungu anataka wafanye, nao humtii yeye kuwa Mtawala kuliko wanadamu. (Mdo. 5:29) Tuna hakika kwamba Yehova atawaongoza watumishi wake hata kama hatua kali ya kisheria itachukuliwa.

Katika miaka michache iliyopita, ndugu katika Jamhuri ya Georgia wamepoteza mali zao, wametendewa kikatili na watu wenye ghasia, na vichapo vyao vimeteketezwa. Lakini hakuna silaha iliyofanywa juu yao ambayo imefanikiwa. (Isa. 54:17) Katika mwaka wa utumishi wa 2004, Mashahidi wa Yehova waliandikishwa kisheria tena nchini Georgia. Makusanyiko yalifanywa bila kuingiliwa, na vichapo vinaingizwa nchini humo bila shida. Kulikuwa na kilele kipya cha wahubiri na cha watu waliohudhuria Ukumbusho.

Huko Armenia, Eritrea, Jamhuri ya Korea, Rwanda, na Turkmenistan, baadhi ya ndugu wamefungwa kwa sababu ya imani yao. Ingawa wanadhulumiwa, wanajua yale ambayo Maandiko yanasema kuhusu sababu ya majaribu yao, jambo linalowasaidia kudumisha utimilifu huku wakimngojea Yehova awakomboe.—1 Pet. 1:6; 2 Pet. 2:9.

Unaposoma Matukio Muhimu ya Mwaka Uliopita na kuchunguza Ripoti ya Ulimwenguni Pote ya Mwaka wa 2004, utafurahia wema wa Yehova. (Zab. 31:19; 65:11) Ni matumaini yetu kwamba Kitabu cha Mwaka cha 2005 kitakutia moyo uendelee kutembea kwa njia inayomfurahisha Mungu.—1 The. 4:1.

Jitihada kubwa bado zinafanywa ili kuwahubiria watu wa aina zote ile kweli. Kwa mfano, video, diski za DVD katika lugha ya ishara, na vifaa vingine kwa ajili ya viziwi, na vichapo katika maandishi ya vipofu vimetayarishwa ili kuwasaidia kiroho wale wasioweza kusikia na wasioweza kuona. Wahubiri wengi wa Ufalme wamejifunza lugha zinazozungumzwa na wahamiaji wanaoishi katika eneo la kutaniko lao.

Isitoshe, maelfu ya vikundi vimeanzishwa katika maeneo yasiyofikika kwa urahisi. Ofisi moja ya tawi inashughulikia vikundi 300 ambavyo vina wahubiri zaidi ya 7,000. Kuna tumaini kubwa kwamba vikundi hivyo vitakuwa makutaniko! Zaidi ya hayo, kati ya watu 16,760,607 waliohudhuria Ukumbusho, zaidi ya milioni 10 si Mashahidi. Kwa hiyo, yaelekea kwamba bado kuna mavuno mengi.

Tunamshukuru Yehova kwa baraka zake nyingi na kwa jinsi anavyotutunza kwa upendo siku baada ya siku. (Met. 10:22; Mal. 3:10; 1 Pet. 5:7) Tunaposonga mbele kwa umoja katika ‘siku hizi za mwisho,’ tunamtumaini na kumtegemea Yehova. Hata tupatwe na matatizo gani, na tukumbuke andiko letu la mwaka wa 2005: “Msaada wangu unatoka kwa Yehova.” (Zab. 121:2) Tafadhali mwe na hakika kwamba tunawapenda na tunasali kwa ajili yenu.

Ndugu zenu,

Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki