Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 12/15 uku. 30
  • Je! Wewe Unakumbuka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Unakumbuka?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • ‘Nendeni Mkafanye Wanafunzi, Mkiwabatiza’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Kuwasiliana na Ulimwengu wa Roho—Kunaonwaje na Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 12/15 uku. 30

Je! Wewe Unakumbuka?

Je! wewe umepata yale matoleo ya juzijuzi ya Mnara wa Mlinzi kuwa yenye thamani iliyo na mafaa kwako? Basi kwa sababu gani usijaribu kumbukumbu lako kwa yanayofuata:

◻ Kwa sababu gani Timotheo alikuwa mfano mzuri sana kwa vijana kufuata?

Timotheo alidhabihu yanayoitwa maisha ya kikawaida ya kukaa nyumbani ili awe mwandamani mwenye kutegemeka na aliye mwaminifu wa Paulo. Yeye alishikamana na Paulo nyakati nzuri na mbaya, akimtegemeza katika ile kazi ya kuhubiri na kuwa mwenye nia ya kutumikia mahali po pote alipotumwa. (Wafilipi 2:19, 20)—8/15, ukurasa 14.

◻ Ni nini zile sifa zinazotakwa kwa ubatizo?

Mtaka-ubatizo lazima afikirie kwa ufahamu mambo yanayohusika. Lazima yeye kwa kweli atake kutumikia Yehova kwa sababu anampenda Yeye. Yeye anaonyesha hilo kwa kushika sana matakwa ya kiadili ya Mungu na kushiriki imani yake pamoja na wengine. Yeye pia anahitaji kufanya wakfu wa kibinafsi kwa Yehova katika sala.—8/15, ukurasa 16.

◻ Kwa sababu gani ni kosa kufanya upelelezi ili kuona jinsi yalivyo mawasiliano na ulimwengu wa roho?

Kupeleleza mawasiliano na ulimwengu wa roho ni sawa na kupenda kile ambacho Yehova anachukia. (Mithali 6:16-19) Kwa kweli, huko ni kama kukataa Yehova na kwenda upande mmoja na adui mkuu zaidi wa Mungu na wafuasi wa huyo. —9/1, ukurasa 5.

◻ Ni nini kile “kitabu cha ukumbusho” kinachosemwa katika Malaki 3:16?

Kutoka wakati wa Abeli na kuendelea mbele, Mungu amekuwa akiona, kana kwamba anaandika katika kitabu, wale wa aina ya wanadamu wenye kukomboleka ambao wanastahili kukumbukwa kwa habari ya uzima wa milele. Hiki “kitabu cha ukumbusho” ni sawa na “kile kitabu cha uzima” na “ile hatikunjo ya uzima.”(Ufunuo 3:5; 17:8, NW; Mathayo 23:35;)—9/1, ukurasa 29.

◻ Ni jambo gani ambalo linafanya rafiki wa kweli awe mwenye thamani kubwa?

Wewe unaweza siku zote kugeukia rafiki wa kweli kwa msaada, shauri, faraja, na uandamani mchangamfu.​—9/15, kurasa 3,4.

◻ Ni nini ile “hewa” yenye kufisha ya ulimwengu huu?

Ni ile roho ya ujumla, au mwelekeo mkuu unaotawala wa ubinafsi na kutotii, ambao unaonyeshwa na watu waliotenganishwa mbali na urafiki na Mungu. (Waefeso 2:2; 1 Wakorintho 2:12)—9/15, ukurasa 11.

◻ Ili dini iwe yenye thamani yenye mafaa ni lazima ifanye nini?

Ni lazima hiyo izae tunda jema. Ni lazima itokeze watu bora. Ni lazima iweze kueleza sababu inayofanya mambo yawe kama yalivyo leo duniani. Na inapaswa kukaza kikiki katika akili na mioyo ya watu tumaini hakika kwa wakati ujao. (Mathayo 7:17-20)—10/1, ukurasa 7.

◻ Ni mambo gani ambayo ule Mgeuzo Mkuu ulishindwa kutimiza?

Wafanya-mgeuzo fulani wa mapema walikuwa wametazamia sana kurudi kwenye viwango vya Biblia, kwenye Ukristo unaotakata. Tazamio hilo halikutimizwa kamwe. Wakati ulipoendelea kupita, mafundisho ya msingi ya makanisa ya Kiprotestanti, yawe ni makanisa ya kitaifa au mengineyo, yalipatana kwa sehemu kubwa na yale ya Kanisa Katoliki la Roma.—10/1, ukurasa 25.

◻ Ni jambo gani ambalo liliongoza kwenye hukumu kali ya Mungu juu ya Musa na Haruni kufuatia kile kisa cha kule Kadeshi-barnea?

Zaburi 106:32,33 inatoa mwono wa ndani katika kisa hicho, ikionyesha kwamba Musa alitenda kwa kuongozwa na roho yenye uchungu ‘akisema haraka-haraka kwa midomo yake.’ (NW) Kwa maneno ya hasira, yeye alivuta fikira kwake mwenyewe na Haruni badala ya kuzivuta kwa Yehova, ambaye kwa kweli ndiye angeweza kuandaa maji kimwujiza. Kwa njia hiyo Musa alishindwa ‘kutakaza Mungu mbele za macho ya wale watu.’ (Hesabu 27:12-14, NW) — 12/15, ukurasa 31.

◻ Ni kusudi gani lililotukuka ambalo lilitumikiwa na Sheria ya Mungu iliyopewa kwa Israeli?

Ile Sheria ilipewa kwa Israeli ili kuendeleza lile taifa likiwa safi kimwili, kiroho, kiakili, na kiadili.​—11/1, ukurasa 12.

◻ Ni nini baadhi ya misaada ya kudumisha useja safi?

Sali kwa ukawaida kuomba roho ya Mungu na msaada wake ili kuonyesha tunda layo. Fikiria sana na utumie shauri katika Neno la Mungu. Epuka pornografia na vitumbuizo visivyo vya adili. Jikinge na mashirika yako. Epuka kabisa usemi wote usio safi na mizaha ya maneno machafu.​—11/15, ukurasa 20.

◻ Ni tofauti gani za maana zilizopo kati ya maponyo yaliyoripotiwa katika Biblia na yale ambayo yanaripotiwa na waponyaji-kwa-imani leo?

Yesu na wanafunzi wake hawakutoza kamwe malipo kwa maponyo yao. Maponyo ambayo yalifanywa nyakati za Biblia yalikuwa ama ya papo hapo ama yalitimizwa katika kipindi kifupi cha wakati,—12/1, kurasa 4, 5.

◻ Ni nini baadhi ya manufaa za kuimba kwa sauti kubwa katika ibada ya kweli?

Mhusiko wetu wa kibinafsi katika ibada ya peupe unakuwa wenye nguvu zaidi. Kuimba kunatoa ushuhuda mzuri kwa wapya wenye kuja. Jambo la maana zaidi ya yote, sifa kubwa zaidi inaletwa kwa Yehova.​—12/1, ukurasa 27.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki