Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/90 uku. 7
  • Kufundishwa na Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kufundishwa na Yehova
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Habari Zinazolingana
  • Shule Inayotuzoeza Kufanya Kazi Muhimu Zaidi Maishani
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Shule Yenye Mafanikio Ambayo Ni ya Ulimwenguni Pote
    Amkeni!—1995
  • Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 2015 Itatusaidia Kuboresha Ufundishaji Wetu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Kutayarisha Migawo ya Shule
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 12/90 uku. 7

Kufundishwa na Yehova

1 Nabii Isaya alijulisha wazi hivi: “Bwana MUNGU [Yehova, NW] amenipa ulimi wa hao wafundishwao, nipate kujua jinsi ya kutegemeza kwa maneno yeye aliyechoka.” (Isa. 50:4) Njia moja Yehova afanyavyo hivyo ni kupitia mazoezi yanayoandaliwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Ingawa hivyo, jitihada za watu mmoja mmoja zingali zatakiwa. Kiongozi cha Shule ya Huduma ya Kitheokrasi katika ukurasa wa 39 huonelea hivi: “Bila kujali mara ambazo umeshughulika na namna fulani ya mgawo, sikuzote kutayarisha ni kwa faida.” Hiyo yatuhusu sisi sote, iwe tumekuwa katika shule hiyo kwa miezi michache tu au tangu shule hiyo ilipoanza katika 1943.

2 Wanafunzi wote wapaswa kutayarisha kikamilifu. Hiyo yatia ndani kufikiria wakati. Maagizo katika Ratiba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi hutaarifu hivi: “Kusiwe hotuba ya kuzidi wakati.” Ndugu anayeshughulikia Mgawo Na. 1 anapokuwa na mazoea ya kupitisha wakati, apaswa kupewa ushauri wa faragha. Mwangalizi wa shule apaswa pia kuanza mkutano kwa wakati barabara na kufuata maagizo kuhusu wakati uliogawiwa kwa ajili ya ushauri na maneno yake. Tafadhali angalia kwamba chapa ya 1990 iliyosahihishwa ya kitabu “All Scripture” ndiyo itatumiwa.

3 Wote waweza kunufaishwa sana na sehemu ya mambo makuu ya Biblia. Tunakumbushwa kwamba hayo hayapasi kuwa pitio tu la habari iliyogawiwa. Msemaji apaswa kusaidia wasikilizaji wathamini kwa nini na jinsi habari ilivyo ya thamani kwetu.

4 Vikao vingi vimetumiwa kwa Hotuba Na. 3, kwa mafanikio yenye kutofautiana. Lakini kukumbuka mojapo makusudi makuu ya shule, ambalo ni kutusaidia tutoe kweli kwa usahihi na kwa wazi, inapendekezwa kwamba vikao vihusu utumishi wa shambani au ushahidi wa vivi hivi.

5 Hotuba Na. 4, inapotolewa kutoka kitabu Kupata Faida Zote za Ujana Wako, itagawiwa wanafunzi wapya au walio wachanga zaidi. Bila shaka, mwanafunzi aliyegawiwa apaswa awe aweza kusoma. Hotuba hizo zitatolewa kwa zamu juma kwa juma habari nyingine ikitoka katika kitabu Kutoa Sababu. Katika hotuba zote mbili Hotuba Na. 3 na Hotuba Na. 4, mwanafunzi apaswa kutumia kichwa kilichoonyeshwa.

6 Uangalifu wahitaji kutumiwa inapohusu kutumia habari ya ziada. Baadhi ya habari iliyogawiwa huenda ikahusu fungu moja au mawili tu. Lakini habari hiyo ingali yaweza kutolewa kwa matokeo mazuri katika wakati uliogawiwa kwa kusoma na kufafanua Maandiko, kutumia vielezi, na kadhalika. Kwa ujumla, hatuhitaji kutumia habari iliyo nje ya ile iliyogawiwa. Wasikilizaji wapaswa waweze kufuatana nawe katika kichapo ambacho ndicho msingi wa hotuba yako.

7 Mungu tunayeabudu huandaa chanzo cha hekima na maarifa kisichokwisha. (Rum. 11:33) Hata baada ya mileani za wakati, tutakuwa tungali na mengi ya kujifunza. Uwezo wetu wa kusifu Baba yetu wa kimbingu na kushughulika na matatizo ya maisha pamoja na kuridhika kwetu na shangwe, yote hayo yataongezeka kwa kadiri ya jitihada tunayotumia kupata hekima ya kimungu. Lifanye kuwa azimio lako kunufuaishwa kikamili na uandalizi ambao Mfunzi wetu Mkuu amefanya kwa ajili yetu kwa kuhudhuria kwa ukawaida Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Bidii yako yenye kuendelea katika kutayarisha na kushiriki katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi wakati wa 1991 na ikusaidie kutimiza hilo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki