Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/93 uku. 6
  • Kukubali, Kutumia, na Kunufaika na Neno la Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kukubali, Kutumia, na Kunufaika na Neno la Mungu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Habari Zinazolingana
  • Kuchukua Furushi Letu Wenyewe la Daraka
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Endelea Kulinda Jinsi Utembeavyo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1993
km 3/93 uku. 6

Kukubali, Kutumia, na Kunufaika na Neno la Mungu

1 Ijapokuwa mamilioni ya watu wana nakala ya Biblia, wengi hawaikubali kuwa Neno la Mungu, wengi zaidi hawatumii shauri layo lenye hekima, na hivyo ni wachache hunufaika nayo. Hata hivyo, watu wa Yehova wanaamini kikweli kwamba hiyo ni Neno la Mungu na lafaa kwa mambo yote. (2 Tim. 3:16, 17) Hivyo, kichwa cha programu ya kusanyiko la mzunguko la mwaka wa utumishi wa 1993 kitakuwa “Kukubali, Kutumia, na Kunufaika na Neno la Mungu.”

2 Kutakuwako hotuba, maonyesho, maigizo, mambo yaliyoonwa, na mahoji ya kututia moyo, ya kutusaidia tukuze kwa kina kirefu uthamini wetu kwa Neno la Mungu, na kutusaidia tulitumie kikamili zaidi katika kila upande wa maisha. Programu ya Jumamosi alasiri itakazia shauri na nidhamu katika kifungo cha familia ikihusu tafrija, mashirika, na ufuatiaji mali. Itaonyesha jinsi tunavyopaswa kuwa tofauti na ulimwengu na si kuchukua vitabia vyao vibaya na lugha yao isiyo na heshima au yenye matusi. Kwa kuongezea, kitia-moyo kitatolewa kuwanufaisha wazazi wasio na wenzi wa ndoa na watoto wasio na baba.

3 Pia, watu wapya waliojiweka wakfu watapata fursa ya kubatizwa baada ya kusikiliza hotuba ya Kimaandiko kuhusu habari hiyo siku ya Jumamosi. Wale wanaopanga kubatizwa kwenye kusanyiko la mzunguko wanapaswa kumjulisha mwangalizi msimamizi wa kundi upesi iwezekanavyo ili awe na wakati wa kutosha kupanga na wazee warudie maswali ya wanaotaka kubatizwa.

4 Programu ya Jumapili asubuhi itachunguza njia ambazo kwazo twaweza kujitofautisha wenyewe na ulimwengu kwa kupatanishwa na Neno la Mungu. Umuhimu wa jinsi tunavyoonekana na jinsi ya kuepuka kufisidi akili yetu ni baadhi ya habari itakayochunguzwa. Jumapili alasiri, mwangalizi wa wilaya atatoa hotuba ya watu wote yenye kichwa “Ni Nini Kinachoitofautisha Biblia Kuwa Asilia?” Tunataka kuhakikisha tunawaalika watu wote wenye kupendezwa kwenye programu hiyo nzuri.

5 Tarehe na mahali pa programu hiyo ya kusanyiko la mzunguko itatolewa na mwangalizi wa mzunguko wenu na twawatia moyo wote wahudhurie ili wakubali, watumie, na kunufaika kutokana na shauri la Neno la Mungu.—Yak. 1:22-25.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki