Mipango Yako ya Desemba Ni Nini?
Tunapofikiria juu ya Desemba, tunafikiria juu ya halihewa yenye ujoto, mipango ya kuhudhuria mkusanyiko wa wilaya, na mipango ya pumziko la likizo au matembezi yenye kupendeza kwa watu wa ukoo na marafiki. Unapofanya mipango yako ya Desemba, hapa pana vikumbusha vichache ambavyo vitakusaidia utangulize masilahi ya Ufalme:
◼ Fanya mipango dhahiri ya kuhudhuria mkusanyiko wa wilaya. Panga usafiri na mahali pa kulala mapema iwezekanavyo ili uepuke matatizo yoyote.
◼ Ukienda likizoni, panga kuhudhuria mikutano ya kutaniko la mahali hapo na kushiriki katika huduma. Hakikisha umeleta ripoti zako za utumishi; ikiwezekana zitume kwa posta kwa mwandishi wa kutaniko lako.
◼ Kutembelea watu wa ukoo wasio katika kweli huenda kukakupatia nafasi ya kutoa ushahidi wa vivi hivi wenye matokeo. Hakikisha umebeba Biblia yako na ugavi wa fasihi.
◼ Je, umefikiria juu ya kusaidia kutaniko la karibu linalohitaji msaada wa kutimiza eneo lalo? Zungumza na wazee au mwangalizi wa mzunguko upate habari kuhusu mahitaji ya sehemu hiyo.
◼ Likizo za shule huandaa fursa bora kwa vijana kuongeza utendaji wao wa utumishi. Vijana, je, mwaweza kujiandikisha muwe mapainia-wasaidizi?
◼ Kukiwa na halihewa nzuri, huenda ukaona kwamba utapata matokeo bora kutoa ushahidi mwingi jioni wakati watu wengi wanapokuwa nyumbani.
◼ Wazee wapaswa kuwa chonjo kuweka mipango ya kutaniko katika mpango mzuri, wakipanga mtu fulani atunze madaraka ya wale ambao hawatakuwako.
Kumbuka kwamba “mipango ya mwenye bidii kwa hakika huielekea manufaa.” (Mit. 21:5, NW) Panga kutumia vilivyo fursa zako za kitheokrasi za Desemba.