Mikutano Ya Utumishi Kwa Novemba
Juma Linaloanza Novemba 4
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Taja juu ya ripoti ya utumishi wa shambani ya Agosti ya nchi na ya kutaniko la kwenu.
Dak. 15: “Je, Unalitumia Neno la Mungu Sawasawa?” Maswali na majibu. Tia ndani maelezo kuhusu “Sababu za Kutufanya Tuichunguze Biblia,” kutoka kitabu Kutoa Sababu, kurasa 40-42.
Dak. 20: “Hii Yamaanisha Uhai Udumuo Milele.” (Mafungu 1-5) Baada ya maelezo mafupi ya kufungua kwenye fungu la 1, panga uwe na watangazaji wawili hodari waonyeshe utoaji katika mafungu 2-5. Tia mkazo mradi wa kuanzisha funzo la Biblia.
Wimbo 128 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 11
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.
Dak. 20: Kwa Nini Tumtolee Yehova? Mazungumzo kati ya wazee wawili, wakikazia mambo makuu katika makala kwenye kurasa 28-31 za Mnara wa Mlinzi, Desemba 1, 1995, “Hizo Pesa Hutoka Wapi?” na sanduku lenye kichwa “Jinsi Ambavyo Wengine Hutoa Upaji Kwa Ajili Ya Kazi ya Kuhubiri Ufalme.”
Dak. 15: “Hii Yamaanisha Uhai Udumuo Milele.” (Mafungu 6-8) Zungumzia manufaa za kutumia mfikio wa moja kwa moja kuanzisha mafunzo. Panga uwe na watangazaji wenye uzoefu watoe wonyesho kwa utoaji mbalimbali ulio katika mafungu 6-7. Alika wasikilizaji wasimulie visa vinavyohusu funzo lililoanzishwa katika ziara ya kwanza. Alipotolewa funzo moja kwa moja, mtu mmoja alijibu: “Ndiyo. Njoo ndani. Ningependa kuwa na funzo.” Funzo lilianzishwa, familia yake yote ikashiriki juma lililofuata, na upesi wote wakawa wanahudhuria mikutano na kushiriki kazi ya kuhubiri. Tia moyo wote walete nakala zao za nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Juni 1996 kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma lijalo.
Wimbo 129 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 18
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Pitia Mipango ya utumishi wa shambani juma linalokuja.
Dak. 15: “Tuna Utume.” Maswali na majibu. Toa maelezo kifupi kuhusu mafungu 13-16 katika Mnara wa Mlinzi, Januari 1, 1988, kurasa 28-29.
Dak. 20: Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo. Hotuba itolewe na mwangalizi wa utumishi. Tumekuwa tukitumia kitabu Ujuzi katika kazi ya funzo la Biblia kwa karibu mwaka mmoja. Yamkini wanafunzi kadhaa wamekimaliza tayari, ilhali wengine wamesonga mbele katika kitabu hicho. Tulitiwa moyo tukazie fikira kuongoza mafunzo yanayokusudiwa kusaidia wapya wajifunze kweli haraka, kuitumia katika maisha zao, na kuwa sehemu ya kutaniko. Nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Juni 1996 iliandaa madokezo ya kutusaidia tuwe wafundishaji wenye matokeo. Pitia kifupi baadhi ya mambo tunayoweza kufanya kufundisha wanafunzi kwa ustadi, kama inavyoonyeshwa kwenye mafungu 3-13 ya nyongeza hiyo. Kisha, kazia fikira juu ya jambo linalohitaji kufanywa ili kuwasaidia wachukue msimamo unaofaa, kama ionyeshwavyo katika mafungu 14-22. Soma mafungu 15, 17, 20-21. Pitia baadhi ya ripoti chanya kuonyesha jinsi matokeo mazuri yamepatikana na watangazaji wa kwenu. Tia moyo wengi zaidi washiriki katika kazi ya funzo la Biblia.
Wimbo 85 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 25
Dak. 8: Matangazo ya kwenu na Mahali pa Kulala pa Mwangalizi wa Mzunguko.
Dak. 15: “Mipango Yako ya Desemba Ni Nini?” Hotuba itolewe na mzee.
Dak. 10: Sanduku la Swali. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji.
Dak. 12: Pitia Toleo la Fasihi kwa Desemba. Toa New World Translation pamoja na kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? Ukitumia kurasa 327-331 katika kitabu “Kila Andiko,” onyesha ubora wa New World Translation: Hiyo huinua na kutukuza jina la Mungu (mafungu 1-2); tafsiri zayo bora hufanya andiko lieleweke vizuri zaidi (fungu la 6); ni chombo chenye nguvu zaidi kutumia katika huduma (mafungu 22-23). Onyesha na utoe wonyesho mfupi wa utoaji, ukitumia mawazo yaliyo kwenye ukurasa 189 wa kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? Mahali popote ambapo kupendezwa kwaonyeshwa, mipango hususa yapaswa kufanywa ya ziara ya kurudia.
Wimbo 180 na sala ya kumalizia.