Vikumbusha vya Ukumbusho
Mwadhimisho wa Ukumbusho mwaka huu utafanywa Jumapili, Aprili 8. Wazee wapaswa kuzingatia mambo yafuatayo:
◼ Mnapopanga saa za mkutano, hakikisheni kwamba mifano haitapitishwa mpaka baada ya jua kushuka.
◼ Kila mtu, kutia ndani msemaji, apasa kujulishwa saa na mahali hususa pa sherehe.
◼ Matayarisho ya mkate na divai inayofaa yapasa kufanywa mapema.—Ona Mnara wa Mlinzi, Machi 1, 1985, ukurasa wa 17.
◼ Sahani, bilauri, meza, na kitambaa cha meza kifaacho vyapasa kuletwa kwenye jumba na kuwekwa mahali pake mapema.
◼ Jumba la Ufalme au mahali pengine pa mkutano huo papasa kusafishwa kikamili mapema.
◼ Wakaribishaji na watakaopitisha mifano wapasa kuteuliwa na kuelezwa mapema juu ya utaratibu unaofaa na juu ya wajibu wao.
◼ Mipango yapasa kufanywa kuwatumikia wowote kati ya watiwa-mafuta walio wagonjwa ambao hawawezi kuwapo.
◼ Makutaniko zaidi ya moja yanaporatibiwa kutumia Jumba la Ufalme lilelile, kwapaswa kuwe na makubaliano mazuri miongoni mwa makutaniko ili kuepuka msongamano usio wa lazima kwenye jumba, nje ya jumba na kwenye maegesho ya magari.