Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/05 uku. 1
  • Tenda Mema na Uwe Mkarimu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tenda Mema na Uwe Mkarimu
  • Huduma ya Ufalme—2005
  • Habari Zinazolingana
  • Endeleeni Kujengana
    Huduma ya Ufalme—2005
  • ‘Iweni Wakarimu, Tayari Kushiriki’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • ‘Wakumbuke Maskini’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • “Kuwa Tayari kwa Kila Kazi Njema”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2005
km 4/05 uku. 1

Tenda Mema na Uwe Mkarimu

1 Dorkasi “alizidi katika matendo mema na zawadi za rehema.” (Mdo. 9:36, 39) Yehova Mungu na pia watu waliomfahamu Dorkasi walimpenda kwa sababu ya ukarimu wake. Waebrania 13:16 linasema hivi: “Msisahau kutenda mema na kushiriki vitu pamoja na wengine, kwa maana Mungu hupendezwa vema na dhabihu za namna hiyo.” Tunawezaje kutenda mema na kuwa wakarimu?

2 Njia moja ya kuwanufaisha wengine ni kuwapa ‘vitu vyetu vyenye thamani.’ (Met. 3:9) Michango yetu kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote inatumiwa kwa ajili ya ujenzi wa Majumba ya Ufalme, Majumba ya Kusanyiko, na ofisi za tawi kotekote duniani. Ukarimu wetu umewawezesha mamilioni ya watu kunufaika na mafundisho na ushirika wa kiroho.

3 Wafariji Wengine: Wakati wa msiba, watu wa Yehova huwa tayari ‘kuwatendea mema’ waamini wenzao na watu ambao si Mashahidi. (Gal. 6:10) Baada ya kiwanda kimoja cha kemikali kulipuka nchini Ufaransa, mtu mmoja na mke wake walisema hivi: “Ndugu zetu Wakristo walifika mara moja ili kusaidia kuondoa vifusi katika nyumba yetu na katika nyumba za majirani wetu pia. Majirani wetu walishangaa kuona kwamba watu wengi walikuja kusaidia.” Dada mwingine aliongeza: “Wazee wote walikuja kutusaidia. Walikuja kututia moyo. Huo ndio msaada tuliohitaji zaidi kuliko msaada wa kimwili.”

4 Ijapokuwa kuna njia nyingi za kuwasaidia majirani wetu, njia bora ya kuwasaidia ni kuwaeleza kuhusu kweli inayohusisha “tumaini la uzima wa milele” ambao Yehova mwenyewe ameahidi. (Tito 1:1, 2) Ujumbe wa Biblia unawafariji sana wale wanaohuzunishwa na hali za ulimwengu na dhambi zao wenyewe. (Mt. 5:4) Na tuwe wakarimu na tuwatendee wengine mema tunapokuwa na uwezo wa kufanya hivyo.—Met. 3:27.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki