Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/07 uku. 4
  • Je, Uko Tayari kwa Ajili ya Msiba wa Asili?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Uko Tayari kwa Ajili ya Msiba wa Asili?
  • Huduma ya Ufalme—2007
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Umejitayarisha?
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2020
  • Wasaidie Wengine Wavumilie Nyakati Ngumu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • Sanduku La Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Pambano la Mwanadamu Dhidi ya Misiba
    Amkeni!—1995
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2007
km 1/07 uku. 4

Je, Uko Tayari kwa Ajili ya Msiba wa Asili?

1. Kwa nini ni jambo la hekima kujitayarisha kwa ajili ya misiba?

1 Kila mwaka, mamilioni ya watu ulimwenguni pote, kutia ndani akina ndugu na dada zetu, huathiriwa na matetemeko ya nchi, tsunami, upepo mkali sana, tufani, vimbunga, na mafuriko. Kwa kuwa misiba ya asili hutokea bila kutarajiwa na inaweza kumwathiri mtu yeyote, ni jambo la hekima kujitayarisha.—Met. 21:5.

2. Kwa nini ni muhimu kuwajulisha wazee mahali tunapoishi na namba zetu za simu za karibuni zaidi?

2 Kabla ya Msiba: Nyakati nyingine wenye mamlaka hufaulu kutoa maonyo kuhusu misiba inayokaribia. Ni muhimu kuzingatia maonyo hayo. (Met. 22:3) Chini ya hali hizo wazee watajaribu kuwasiliana na wote katika kutaniko na kuwasaidia kufanya matayarisho yanayohitajika. Baada ya msiba, wazee watajaribu pia kuwasiliana na wote wanaoshirikiana na kutaniko kuona ikiwa wako salama na kuamua ni msaada gani unaohitajika. Wakati muhimu unaweza kupotea ikiwa wazee hawajui jinsi wanavyoweza kuwasiliana na washiriki wa kutaniko. Kwa hiyo, ni muhimu kwa wahubiri kumjulisha mwandishi na mwangalizi wa funzo la kitabu mahali wanapoishi na namba zao za simu za karibuni zaidi.

3. Tunaweza kushirikianaje na wazee ikiwa tunaishi katika eneo ambalo misiba hutokea mara kwa mara?

3 Ikiwa kutaniko liko katika eneo ambalo misiba hutokea mara kwa mara, huenda wazee wakawaomba wahubiri wawape jina na namba ya simu ya mtu wa ukoo au rafiki anayeishi nje ya eneo hilo ambaye wanaweza kuwasiliana naye kunapokuwa na hali ya dharura. Hilo litawawezesha wazee kujua mahali ambapo wanaweza kuwapata wale wanaoondoka eneo lililoathiriwa. Huenda pia wazee wakapanga kuwe na mpango wa kushughulikia hali ya dharura kwa ajili ya kutaniko. Mpango huo unaweza kutia ndani orodha ya vitu ambavyo mtu anapaswa kuhifadhi kwa ajili ya wakati wa dharura, mipango ya kuhamisha watu, na mipango ya kuwasaidia walio na mahitaji ya pekee. Ni muhimu kushirikiana na wazee kufuata mipango hiyo iliyotayarishwa kwa upendo.—Ebr. 13:17.

4. Tunapaswa kufanya nini kunapokuwa na msiba katika eneo letu?

4 Baada ya Msiba: Unapaswa kufanya nini msiba unapotokea katika eneo lenu? Hakikisha kwamba familia yako imeandaliwa mahitaji yake ya kimwili. Kadiri uwezavyo, wasaidie wengine walioathiriwa. Jitahidi kuwasiliana na mwangalizi wa funzo lenu la kitabu au mzee mwingine haraka iwezekanavyo. Unapaswa kufanya hivyo hata ikiwa uko salama na huhitaji msaada. Ikiwa unahitaji msaada, uwe na hakika kwamba ndugu zako wanafanya yote wawezayo kukusaidia. (1 Kor. 13:4, 7) Kumbuka kwamba Yehova anaelewa hali yako; mtegemee ili akutunze. (Zab. 37:39; 62:8) Uwe macho kuona nafasi za kuwasaidia wengine kiroho na kihisia. (2 Kor. 1:3, 4) Rudia utendaji wako wa kitheokrasi haraka iwezekanavyo.—Mt. 6:33.

5. Tukiwa Wakristo tunaathiriwaje na uwezekano wa kutokea kwa misiba?

5 Ingawa ulimwengu una wasiwasi mwingi kuhusu kutokea kwa msiba, tunaweza kutazamia wakati ujao tukiwa na uhakika. Hivi karibuni misiba haitakuwapo tena. (Ufu. 21:4) Kwa wakati huu, tunaweza kuchukua hatua fulani ili kujitayarisha kwa ajili ya wakati wa taabu na hali ngumu huku tukiendelea kudumisha bidii ya kuwatangazia wengine habari njema.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki