Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/11 uku. 7
  • Wazoeze Watoto Wako Kuwa Wahudumu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wazoeze Watoto Wako Kuwa Wahudumu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Habari Zinazolingana
  • Kujenga Familia Yenye Nguvu Kiroho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Wazazi—Wafundisheni Watoto Wenu Tangu Utotoni
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Umewawekea Watoto Wako Miradi Gani?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Kuwalea Watoto Wako Wampende Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2011
km 1/11 uku. 7

Wazoeze Watoto Wako Kuwa Wahudumu

1. Zaburi 148:12, 13 inawahimiza wazazi Wakristo wafanye nini?

1 Yehova anawaalika watoto wamsifu. (Zab. 148:12, 13) Hivyo, wazazi Wakristo wanawafundisha watoto wao kweli za Biblia na sheria za Mungu kuhusu maadili. Vilevile, wanawazoeza kuwa wahudumu wa habari njema. Hilo linaweza kufanywaje hatua kwa hatua?

2. Mfano mzuri wa mzazi unaweza kuwa na matokeo gani kwa watoto wake?

2 Kuwa Mfano Mzuri: Mwamuzi Gideoni aliwaambia wanaume wake 300 hivi: “Jifunzeni kwa kunitazama.” (Amu. 7:17) Kwa kawaida, watoto huwatazama na kuwaiga wazazi wao. Baba mmoja anafanya kazi ya usiku, lakini badala ya kulala anaporudi nyumbani Jumamosi asubuhi, yeye huwapeleka watoto wake katika utumishi ingawa huwa amechoka sana. Bila kusema lolote, anawafundisha watoto wake kwamba huduma inapaswa kutangulizwa. (Mt. 6:33) Je, watoto wako hukuona ukishiriki kwa shangwe sehemu mbalimbali za ibada kama vile kusali, kusoma Biblia, kutoa maelezo, na kuhubiri? Ni kweli kwamba hutakuwa mfano mkamilifu. Lakini watoto wako watathamini zaidi jitihada zako za kuwafundisha kumwabudu Yehova ikiwa wataona bidii yako ya kumtumikia.—Kum. 6:6, 7; Rom. 2:21, 22.

3. Ni miradi gani ya kiroho ambayo wazazi wanaweza kuendelea kuwasaidia watoto wao kuweka na kufikia?

3 Kuendelea Kuweka Miradi: Wazazi huwazoeza watoto wao kutembea, kuzungumza, kujivisha, na mambo mengine bila kuchoka. Watoto wanapofikia umri fulani, wanawekewa miradi mingine. Ikiwa wazazi ni Wakristo, wanawasaidia pia watoto wao kuweka na kufikia miradi ya kiroho kulingana na umri na uwezo wao. (1 Kor. 9:26) Je, unawafundisha watoto wako kutoa maelezo kwa maneno yao wenyewe na kutayarisha hotuba zao wenyewe katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi? (Zab. 35:18) Je, unawazoeza kushiriki katika sehemu mbalimbali za huduma? Unawawekea mradi wa kubatizwa na kuingia katika utumishi wa wakati wote? Je, unawasaidia kushirikiana na waeneza injili wenye shangwe na bidii ambao watawatia moyo?—Met. 13:20.

4. Watoto hunufaikaje wanapokuwa na wazazi ambao huanza kuwazoeza katika huduma wakiwa wangali wachanga?

4 Mtunga-zaburi alisema hivi: “Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu, na mpaka sasa ninaendelea kutangaza kazi zako za ajabu.” (Zab. 71:17) Anza kuwazoeza watoto wako kuwa wahudumu wakiwa wangali wachanga. Bila shaka, msingi wa kiroho ambao unawasaidia kuweka utawanufaisha watakapokuwa watu wazima!—Met. 22:6.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki