Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/12 uku. 7
  • Njia Tano za Kupata Funzo la Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Njia Tano za Kupata Funzo la Biblia
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Wewe Huulizia Watu Wanaotaka Kujifunza?
    Huduma ya Ufalme—2006
  • Je! Unatoa Mafunzo ya Biblia?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Sehemu ya 7—Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Jinsi ya Kumsaidia Mwanafunzi wa Biblia Afikie Hatua ya Ubatizo—Sehemu ya Kwanza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2012
km 10/12 uku. 7

Njia Tano za Kupata Funzo la Biblia

1. Tunapaswa kufanya nini iwapo ni vigumu kupata funzo la Biblia katika eneo letu, na kwa nini?

1 Je, umeona ni vigumu kwako kupata mtu wa kujifunza naye Biblia? Endelea kujitahidi. Yehova huwabariki wale wanaofanya mapenzi yake bila kuchoka. (Gal. 6:9) Mapendekezo matano yafuatayo yanaweza kukusaidia.

2. Tunaweza kutumiaje njia ya moja kwa moja kuanzisha funzo?

2 Njia ya Moja kwa Moja: Watu wengi wanajua kuwa sisi hutoa magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, lakini huenda wasijue kwamba tunajifunza na watu Biblia. Kwa nini tusijaribu njia ya moja kwa moja tunapoenda nyumba kwa nyumba? Pia, unaweza kuwauliza watu wanaopendezwa unaowatembelea kama wangependa kujifunza Biblia. Wasipokubali, unaweza kuendelea kuwaachia machapisho na kuendelea kukuza upendezi. Kwa miaka mingi ndugu mmoja alikuwa akiwatembelea wenzi fulani wa ndoa na kuwaachia magazeti kwa ukawaida. Baada ya kuwaachia magazeti ya karibuni, aligeuka ili aondoke lakini akafikiria na kisha akawauliza: “Je, mngependa kujifunza Biblia?” Alishangaa walipokubali. Sasa wamebatizwa.

3. Je, tunapaswa kufikiri kwamba wanaohudhuria mikutano wanajifunza Biblia na mtu fulani? Eleza.

3 Wanaohudhuria Mikutano: Usifikiri kwamba watu wanaopendezwa unaowaona katika mikutano ya kutaniko tayari wanajifunza Biblia. Ndugu mmoja anasema: “Nusu ya mafunzo niliyokuwa nayo niliyapata kwa kuzungumza na wale waliokuwa wakihudhuria mikutano.” Dada mmoja aliamua kumfikia mwanamke mwenye haya aliyekuwa akihudhuria mikutano pamoja na binti zake waliobatizwa. Mwanamke huyo alikuwa akihudhuria mikutano kwa miaka 15 hivi na sikuzote alifika Jumba la Ufalme mikutano ilipokuwa tu inaanza na kuondoka mara tu ilipoisha. Mwanamke huyo alikubali kujifunza na hatimaye aliingia katika kweli. Dada huyo anaandika: “Nasikitika kwamba nilisubiri kwa miaka 15 ili nimuulize ikiwa angependa kujifunza!”

4. Tunaweza kupataje funzo kwa kuulizia wale wanaotaka kujifunza?

4 Ulizia Wanaotaka Kujifunza: Dada mmoja hujitahidi kuandamana na wengine kwenye mafunzo yao ya Biblia. Kwa ruhusa ya mwalimu, mwishoni mwa funzo humuuliza mwanafunzi ikiwa anajua watu wengine wowote ambao wangependa kujifunza. Unapomtolea kitabu Biblia Inafundisha mtu ambaye umekuwa ukimtembelea, unaweza kumwuliza: “Je, unamjua mtu mwingine yeyote ambaye angependa kupata kitabu hiki?” Nyakati nyingine, hali haziwaruhusu wahubiri na mapainia kujifunza na mtu wanayekutana naye shambani. Hivyo, wajulishe wengine kwamba ungependa kupata funzo la Biblia.

5. Kwa nini tuwaulize wenzi wa ndoa wasio waamini wa washiriki wa kutaniko letu ikiwa wangependa kujifunza?

5 Wenzi wa Ndoa Wasio Waamini: Je, kuna wahubiri katika kutaniko lenu wenye wenzi wasio waamini? Wenzi fulani wa ndoa wasio waamini hukataa kuzungumzia Biblia na wenzi wao Wakristo lakini wanaweza kukubali kujifunza Biblia na watu wengine ambao si wa familia yao. Mara nyingi, ni vizuri zaidi kuzungumza kwanza na mume au mke wa mwenzi asiye mwamini ili kujua njia bora ya kumfikia.

6. Sala ina thamani gani tunapojaribu kutafuta funzo?

6 Sala: Usipuuze nguvu za sala. (Yak. 5:16) Yehova anaahidi kusikiliza maombi yetu yanapopatana na mapenzi yake. (1 Yoh. 5:14) Ndugu mmoja aliyekuwa na ratiba yenye shughuli nyingi alianza kusali ili apate funzo la Biblia. Mke wake alijiuliza ikiwa mume wake angeweza kupata wakati wa kumsaidia mwanafunzi, hasa ikiwa mwanafunzi huyo angekuwa na matatizo mengi. Kwa hiyo alimjulisha Yehova mahangaiko hayo alipokuwa akisali ili mume wake apate funzo. Sala zao zilijibiwa baada ya majuma mawili hivi wakati painia mmoja kutanikoni alipompata mwanamume fulani aliyetaka kujifunza na akampa ndugu huyo funzo hilo. Mke anaandika hivi: “Kwa yeyote anayehisi kwamba hawezi kuongoza funzo la Biblia, ninamwambia hivi: Taja mambo hususa katika sala zako, na usiache kusali. Tumepata shangwe nyingi kuliko nilivyowazia.” Ukiwa mstahimilivu, wewe pia unaweza kupata funzo la Biblia na kujionea shangwe ya kumsaidia mtu fulani kutembea katika “barabara inayoongoza kwenye uzima.”—Mt. 7:13, 14.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki