Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Kutoa Kitabu Biblia Inafundisha
Kwa Nini Ni Muhimu: Kitabu Biblia Inafundisha ni kifaa muhimu cha kufundishia. Lakini, kabla ya kuanza kukitumia kujifunza na mtu anayependezwa, lazima kwanza tumwachie. Kwa hiyo, sote tunapaswa kujitahidi kuwa stadi katika kutoa kitabu Biblia Inafundisha. (Met. 22:29) Kuna mapendekezo mengi, hata hivyo, wahubiri wanapaswa kutumia pendekezo lenye matokeo.
Tumia Dokezo Hili kwa Mwezi Mzima:
Fanyeni mazoezi wakati wa ibada yenu ya familia.
Unapokuwa katika utumishi, waeleze wahubiri wengine utangulizi uliopanga kutumia. (Met. 27:17) Badili utangulizi wako ikiwa hupati matokeo.