Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w09 2/1 uku. 9
  • Je, Mungu Anakubali Dini Zote?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Mungu Anakubali Dini Zote?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Habari Zinazolingana
  • Dini Yako Inapasa Kufikiriwa Sana
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Kwa nini ni Hekima Kuichungaza Dini Yako
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
  • Jinsi ya Kumwabudu Mungu Kwa Njia Inayofaa
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Je! Dini Zote Zawaongoza Watu Kwa Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
w09 2/1 uku. 9

Je, Mungu Anakubali Dini Zote?

Watu wengi wanajibu hivi:

▪ “Dini zote ni njia zinazoongoza kwa Mungu.”

▪ “Maadamu wewe ni mnyoofu si jambo la maana unaamini nini.”

Yesu alisema nini?

▪ “Ingieni kupitia lango jembamba; kwa sababu barabara inayoongoza kwenye uharibifu ni pana na kubwa, na wengi ndio wanaoipitia; lakini lango ni jembamba na barabara inayoongoza kwenye uzima ina nafasi ndogo, na wachache ndio wanaoipata.” (Mathayo 7:13, 14) Yesu hakuamini kwamba barabara zote zinaongoza kwa Mungu.

▪ “Wengi wataniambia siku hiyo, ‘Bwana, Bwana, hatukutoa unabii katika jina lako, na kufukuza roho waovu katika jina lako, na kufanya matendo mengi yenye nguvu katika jina lako?’ na hata hivyo nitawaambia waziwazi: Sikuwajua ninyi kamwe! Ondokeni kwangu, ninyi wenye matendo ya uasi-sheria.” (Mathayo 7:22, 23) Yesu hawakubali wote wanaodai kuwa wafuasi wake.

WATU wengi wa kidini wanashikilia sana imani na mapokeo yao. Lakini, namna gani ikiwa mafundisho hayo hayapatani na Neno la Mungu, Biblia? Yesu alionyesha hatari ya kufuata mapokeo ya wanadamu alipowaambia hivi viongozi wa kidini wa siku zake: “Mmelibatilisha neno la Mungu kwa sababu ya mapokeo yenu.” Kisha akanukuu maneno haya ya Mungu: “Watu hawa huniheshimu kwa midomo yao, bali moyo wao umepelekwa mbali nami. Wao huniabudu bure, kwa sababu wao hufundisha amri za wanadamu kuwa mafundisho.”—Mathayo 15:1-9; Isaya 29:13.

Mwenendo ni muhimu pia, si imani tu. Biblia inasema hivi kuhusu watu fulani wanaodai kumwabudu Mungu: “Wao hutangaza hadharani kwamba wanamjua Mungu, lakini humkana kwa matendo yao.” (Tito 1:16) Kwa kweli, Biblia inasema hivi kuhusu watu wanaoishi katika nyakati zetu: “Watapenda anasa kuliko kumpenda Mungu. Kwa nje wataonekana kama watu wenye kumcha Mungu, lakini wataikana nguvu yake. Jiepushe kabisa na watu wa namna hiyo.”—2 Timotheo 3:4, 5, Biblia Habari Njema.

Unyoofu ni muhimu, lakini mengi zaidi yanahitajika. Kwa nini? Kwa sababu mtu anaweza kuamini kwa unyoofu mambo yasiyo ya kweli. Kwa hiyo, ni muhimu kuwa na ujuzi sahihi kumhusu Mungu. (Waroma 10:2, 3) Kupata ujuzi huo na kutenda kupatana na yale ambayo Biblia inasema kutatusaidia kumpendeza Mungu. (Mathayo 7:21) Hivyo, basi, dini ya kweli inahusisha nia inayofaa, imani inayofaa, na matendo yanayofaa. Na matendo yanayofaa ni kufanya mapenzi ya Mungu kila siku!—1 Yohana 2:17.

Ikiwa ungependa kujua mengi zaidi kuhusu kile ambacho Biblia inatuambia kumhusu Mungu, wasiliana na Mashahidi wa Yehova ili upate funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.

[Blabu katika ukurasa wa 9]

Dini ya kweli inahusisha nia inayofaa, imani inayofaa, na matendo yanayofaa

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki