Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Trakti Habari za Ufalme Na. 38
“Ninashiriki katika kampeni inayoendelea ulimwenguni pote ya kusambaza ujumbe huu muhimu. Hii ni nakala yako.”
Zingatia: Zungumza kwa ufupi ili mmalize eneo lenu. Hata hivyo katika visa vingine, huenda mwenye nyumba akapendezwa kwelikweli hivi kwamba akaomba mwendelee na mazungumzo. Ikiwa ndivyo, unaweza kumuuliza swali ambalo ni kichwa cha trakti hiyo, umsomee jibu la Biblia linalopatikana katika trakti hiyo, na mzungumzie mambo fulani yaliyomo kadiri wakati unavyoruhusu. Kabla ya kuondoka mwonyeshe swali lililo chini ya kichwa “Jambo la Kufikiria” linalopatikana nyuma ya trakti na ufanye mipango ya kurudi ili mlizungumzie swali hilo.
Mnara wa Mlinzi Novemba 1
“Kwa maoni yako, unafikiri ni uwongo gani mkubwa sana ambao watu wamesema kumhusu Mungu? [Mruhusu ajibu.] Kulingana na Biblia, Mungu anataka watu wampende na wamwamini. [Soma Isaya 41:13.] Gazeti hili linazungumzia mambo matatu ya uwongo kumhusu Mungu ambayo yamefanya iwe vigumu kwa watu wengine kumkaribia.”
Amkeni Novemba
“Leo, tunawatembelea kwa muda mfupi tukijua kwamba watu wengi wanahangaishwa sana na kuzorota kwa maadili. Je, unafikiri jamii imechangia kuzorota kwa maadili? [Mruhusu ajibu.] Biblia ilitabiri kwamba mtazamo na tabia za watu zingebadilika. [Soma 2 Timotheo 3:1-5.] Gazeti hili linazungumzia kwa nini tunaweza kuamini viwango vya maadili vilivyomo katika Biblia.”