Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 3/96 uku. 8
  • Tusaidie Wengine Wapate Faida

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tusaidie Wengine Wapate Faida
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tutende Mema kwa Jirani Yetu kwa Kufuatia Kupendezwa Kokote
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Utoaji Mbalimbali Uliopendekezwa kwa Ajili ya Utumishi wa Shambani
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Kufundisha Neno La Mungu Kwa Kutumia Broshua
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Tufurahie Kutoa Ushahidi Kamili
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 3/96 uku. 8

Tusaidie Wengine Wapate Faida

1 Yehova anaahidi kutufundisha yale tunayopaswa kujua. Katika Zaburi 32:​8, anatutolea ahadi hii: “Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayokwenda. Nitakushauri na jicho langu likikutazama.” Uhakika huo ni chanzo cha faida nyingi kwetu. Kwa kujinyima, tunatamani kuonyesha jirani yetu faida gani anazoweza kupata kwa kufuata mashauri yenye hekima ya Biblia (Isa. 48:17) Hilo ndilo tutafanya kwa kutolea kitabu Kuishi Milele katika Machi. Katika matoleo yetu, tunaweza kuonyesha katika njia mbalimbali thamani ya Biblia inayotenda kazi.

 2 Matatizo ya ndoa yakiwa yenye kuenea sana wakati wetu huu, tungeweza kutoa wazo lifuatalo tukitegemea kitabu “Kuishi Milele”:

◼ “Watu wengi ambao nimezungumza nao wanahangaika sana kuona ongezeko lenye kushtusha la matatizo ya ndoa na pia hesabu ya talaka nyingi. Wewe unafikiri nini juu ya hali hiyo? [Acha mtu ajibu.] Watu wengi hawaelewi ni nini sababu kabisa za magumu hayo. Ikiwa wenzi wa ndoa walikuwa tayari kufanya jitihada za kutoka moyoni, wangeweza kuokoa si tu ndoa zao, lakini zaidi ya hilo wangeonja furaha ya kweli. Matumizi ya mashauri yaliyomo katika Biblia yanawezesha kuwa na ndoa yenye furaha.” Tusome Waefeso 5:​28, 29, 33. Tufungue kitabu kwenye ukurasa 243, tuchunguze mafungu 16 na 17, kisha tutolee kitabu.

 3 Watoto wanahitaji kuona wazazi wao wakitumia wakati wakiwa pamoja nao na pia kuangalia malezi yao. Kwa kutolea kitabu “Kuishi Milele,” tungeweza kusema:

◼ “Sisi sote tunapendezwa na wakati ujao wa watoto wetu. Kwa maoni yako, nini iliyo njia bora kwa wazazi kutayarisha watoto wao kwa ajili ya wakati ujao ulio mzuri? [Tuache mtu ajibu.] Tusikilize shauri la kibiblia linalotolewa na mezali hii ya kibiblia iliyoandikwa yapata miaka 3 000. [Tusome Mezali 22:6.] Hata ikiwa watoto wetu wanafaidika sana na elimu wanayopokea shuleni, hata hivyo ni wazazi ambao, nyumbani, wanaowatolea mazoezi yaliyo bora zaidi. Mazoezi hayo yanataka wakati, uangalifu na pia upendo, kwa vyovyote yanastahili kabisa jitihada.” Tufungue kitabu kwenye ukurasa 245 na tuchunguze mafungu 20 na 21. Kisha, tufasirie namna mtu anaweza kukitumia kitabu hicho ili kujifunza Biblia katika familia.

 4 Labda tungependa kutolea kitabu “Kuishi Milele” kwa kufasiria kwamba dunia itageuzwa kuwa paradiso:

◼ “Bila shaka unajiuliza ni maisha ya namna gani wakati ujao unatuandalia. Katika ile sala ya Baba Yetu, Yesu alitufundisha kusali ili kwamba mapenzi ya Mungu yafanyike duniani kama vile yanavyofanyika mbinguni. Basi dunia itafananaje wakati maneno hayo yatakapotimia? [Tuache mtu ajibu.] Tazama picha iliyotengenezwa kwa ufundi ya dunia hiyo ya kiparadiso. [Tuonyeshe picha ya kurasa 12 na 13. Kisha tusome Isaya 11:​6-9, linaloonyeshwa kwenye fungu la 12.] Je! haitakuwa jambo la ajabu kuishi katika makao kama haya? Kitabu hiki kinafasiria yale familia yako na wewe mwenyewe mnatakiwa kufanya ili kuishi katika paradiso hii.”

 5 Ikiwa tunataka kufanikiwa katika mahubiri ya nyumba kwa nyumba ni jambo la lazima kutayarisha mahubiri yetu. Kabla ya kugonga kwenye mlango, tuwe tayari kutoa wazo fulani la kibiblia lililo wazi. Pia tuwe akilini na maelezo mafupi juu ya wazo fulani lenye kuvutia la gazeti au trakti ambayo tunafikiria kutolea ikiwa mtu anakataa kitabu. Katika mwezi wa Machi, tutumie nafasi zote zinazojitokeza ili kupanda zile mbengu za Ufalme. (Muh. 11:6) Kwa kufanya hivyo, tutasaidia majirani zetu kupata faida za milele.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine