Tutende Mema kwa Jirani Yetu kwa Kufuatia Kupendezwa Kokote
1 Ni kwa msingi gani tunaamua kumuachia msikilizaji fulani kitabu? Kanuni ya lazima sana ni: kupendezwa kwake. Ni kwa kutumia kanuni hiyohiyo kwamba tunarudi tena kuwaona watu. Inapoonekana wazi kwamba mtu fulani anapendezwa, hata ikiwa anapendezwa kidogo, na ujumbe wa Ufalme, tunafanya yote tuwezayo ili kumtendea mema. Tunafanya hivyo ziara ya kurudia, tukiwa na tamaa ya kusitawisha kupendezwa kwake na kuanzisha funzo la Biblia. Hilo ndilo kusudi letu hata ikiwa hatuachi kichapo. Tutafanyaje hivyo?
2 Ikiwa mazungumzo yetu yaliyotangulia yalihusu magumu mbalimbali ya ndoa na kwamba tuliacha kitabu “Kuishi Milele,” tungeweza kuanzisha upya mazungumzo kwa kusema:
◼ “Katika ziara yangu iliyotangulia, tulizungumza juu ya ndoa na pia mashauri ya Biblia yanayotenda kazi yanayoweza kutufanya tuwe na furaha. Je! haufikiri kwamba hata familia zilizo nzuri zinakutana wakati mwingine na magumu? [Tuache mtu ajibu.] Biblia inatoa mashauri bora kuhusu namna ya kutatua magumu ya familia. Linaweza kuwa jambo lenye faida kujifunza Biblia katika familia.” Tufungue kitabu kwenye ukurasa 246 na tutoe maelezo juu ya fungu la 23. Tusome Yohane 17:3, na tufanye pendekezo kwa familia kuisaidia kujifunza Biblia nyumbani kwao.
3 Ikiwa tulizungumza kuhusu watoto na pia ulazima wa kuwatolea malezi mazuri, tungeweza kuendelea hivi:
◼ “Tulipoonana mara ya mwisho, tuliweza kufasiria ya kwamba watoto wanapaswa kupata elimu ya kiroho na namna gani wazazi wanaweza kuwatolea hiyo. Wazazi wengi ambao ninakutana nao wanahangaika akilini kwa kuwa vijana wengi leo wanajiendesha vibaya. Na wewe, unafikiri nini juu ya. . . ? [Tutaje mfano moja wa mwenendo mpotovu wa vijana ulio kawaida katika eneo na pia tuache mtu ajibu.] Uniruhusu nikuonyeshe mashauri fulani yanayotenda kazi yapatikanayo katika Biblia.” Tufungue kitabu Kuishi Milele kwenye ukurasa 246, fungu la 22, tuzungumzie wazo kuu na pia tusome Waefeso 6:4. Tuonyeshe kwamba watoto wote wana lazima, kwa vyo vyote, ya nidhamu na pia uongozi na kwamba, wazazi wanapowatolea huo, vijana wanakuwa wenye furaha na wenye heshima zaidi. Tufasirie namna gani sisi tunajifunza Biblia na watoto wetu.
4 Ikiwa mazungumzo yalihusu paradiso ya kidunia, tuamshe upya kupendezwa kwa kusema:
◼ “Tulitazama mojawapo wa picha za kitabu hiki ambazo zinatufanya tuone namna dunia itafanana wakati Mungu ataifanya iwe paradiso. Lakini furaha yetu ingekuwa isiyokamilika ikiwa tungefaidika na paradiso hiyo sisi wenyewe bila wale tuwapendao. Je! hayo si ndio maoni yako? [Tuache mtu ajibu.] Kisha tufungue kitabu Kuishi Milele kwenye ukurasa 162. Tusome Ufunuo 21:3, 4, na tufasirie namna gani wale tuwapendao wataweza kuwa pamoja nasi siku zote. Ikiwa mtu ni mwenye kusikiliza, tusome Yohana 5:28, 29, ili kuonyesha kwamba wafu watarudi kwenye uhai. Kwa kuongoza ishara ya mkono kwenye jalada la kitabu, tuhakikishe kwa kusema: “Hili ni jambo hakika kabisa: inawezekana kuishi milele katika dunia ya kiparadiso!” Tumpe mtu huyo ahadi ya kuonana tena ili kumfasiria kirefu jambo linalotufanya tufikiri kwamba paradiso inakaribia.
5 Kusudi kubwa la kufanya ziara ya kurudia ni lile la kufanya ujumbe wa Ufalme ufaidi watu wanaopendezwa nao. Wachache tu ni wale wasiohitaji kichocheo ili wafikie kufurahia mambo ya kiroho. Tuvutie uangalifu juu ya mawazo kamili yenye kutenda kazi yaliyomo katika vichapo, kwa kukazia ulazima wa kuelewa vizuri Biblia. Tukifikia kusudi hilo wakati wa ziara zetu za kurudia, tutakuwa tumetenda mema kwa jirani yetu kwa njia nzuri iwezekanayo.